Picha ya pamoja kati ya Maafisa wa Ubalozi na Wachezaji
       Mh Balozi John kijazi akikabidhiwa kombe na timu nzima
NA TANZANREP NEW DELHI

Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania [New Delhi] nchini India wiki hii ulifanya hafla kubwa kusherehea ushindi na kuipongeza Timu ya Mpira wa Miguu ya Ubalozi kwa kunyakua Ubingwa wa Mashindano ya  "United Cup 2012" ambayo huzishirikisha Timu za Balozi mbali mbali zilizoko nchini India -  Inter Embassies Soccer Tournament.



Timu ya  ya Ubalozi wa Tanzania iliibuka kidedea  kwa kuifunga Timu ngumu ya Ubalozi wa Botswana magoli 2-0.  Mashindano haya  yalianza rasmi tarehe 29 Machi na kufikia kilele  tarehe  1 Aprili 2012.  



Timu ya Ubalozi  ilijumuisha Familia za Maafisa wa Ubalozi na Wanafunzi wa Tanzania wanosoma katika Jimbo la Delhi pamoja na Majimbo mengine ya jirani.  



Vile  vile, Timu ya Ubalozi ilishinda mechi zote za awali kabla ya kufanikiwa kuingia fainali.  Timu ya Ubalozi wa Botswana ilichukua nafasi ya pili na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Timu ya Ubalozi wa Saudi Arabia.



Balozi nyingine zilizoshiriki katika Mashindano haya ni Denmark, China, Spain, France, Egypt, Saudi Arabia, Indonesia, Netherlands na Israel,  United Nations na Timu ya “Touch of Hope Foundation” na wenyeji  India.



Mashindano haya huandaliwa  "New Delhi United Football Club" kwa kushirikiana na Wadau wengine  kwa madhumuni ya kuimarisha urafiki, Ushirikiano,  upendo na kujenga afya za  washiriki.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Safi sana huu ndio utangazaji halisi wa Nchi yetu naona wahindi walikuwa hawajui Tanzania iko wapi na siku hiyo weng iwao ndio walijua baada ya timu hiyo kuchukuwa kikombe.Hongereni sana Ubalozi na timu nzima kwa ujumla Tangaza Tanzania!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...