Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Ijumaa, Mei 4, 2012, amemteua Bibi Saada Mkuya Salum kuwa Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Uteuzi huo unaanza mara moja.

Rais amefanya uteuzi huo kwa mamlaka aliyo nayo chini ya Ibara ya 66 (i) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, kama ilivyorekebishwa.

Chini ya Ibara hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anapewa mamlaka ya kuteua wabunge 10 kuingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mpaka sasa, Rais Kikwete ameteua wabunge saba. Novemba mwaka 2010, aliteua wabunge watatu na jana, Alhamisi, Mei 3, 2012 ameteua wabunge wengine watatu ambao ni Professa Sospeter Muhongo, Bibi Janet Mbene na Bwana James Mbatia.


Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
4 Mei, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 04, 2012

    Katiba inamruhusu Raisi kuteua Wabunge 10.

    Mwaka 2010 Novemba aliteua Wabunge 7, halafu 2012 Mei, 3 wengine Wabunge 3, halafu tena leo Bibi. Saada Mkuya Salum,

    Sasa wanakuwa 7+3+1=11

    Ameteua Wabunge 11 badala ya 10 hapa inakuwa vipi?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 04, 2012

    Amestuka kuwa aliwasahau vibarakashie wenzie!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 04, 2012

    HIKI NI KATI YA VIFUNGU VINAVYOTAKIWA KUFUTWA KTK KATIBA

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 04, 2012

    Fanyeni haraka mkuu keshamaliza kazi Ikulu..

    David V

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 05, 2012

    Hatimaye James Mbatia amepata ujira wake, kwani anafanya kazi nzuri sana ya CCM kule Upinzani.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 05, 2012

    Wewe ulikuja total 11 soma habari vizuri usikurupuke ka mkojo wa asubuhi

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 05, 2012

    Amevunja katiba, tutamfanyahe huyu mkuu wa kaya? 7+3+1=11

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 05, 2012

    Wewe mdau wa kwanza wacha uzushi.

    Kabla aliteuwa wabunge watatu (Meghji, Shamsi na Mnyaa), juzi watatu (Mbatia, Muhongwa? na Janet) na jana mmoja (Sada).

    Piga jumla ya darasa la kwanza mwenyewe.

    Hao 11 umewatoa wapi? Au amekuchagua wewe hatukupewa taarifa?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...