Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kesho, Jumatatu, Mei 7, 2012, atawaapisha Mawaziri na Naibu Mawaziri ambao aliwateua katika mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri aliyoyatangaza Ijumaa iliyopita Ikulu, Dar es Salaam.
Sherehe hizo za kuapishwa viongozi hao zitafanyika kwenye Viwanja vya Ikulu kuanzia saa 5:30 asubuhi.
Watakaopishwa katika sherehe hizo ni Mawaziri wanane wa zamani walioteuliwa kuongoza wizara nyingine, Mawaziri saba wapya katika Baraza la Mawaziri, Naibu Mawaziri sita waliobadilishwa Wizara pamoja na Naibu Mawaziri 10 wapya kabisa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...