Kampuni ya Michelin ya Ufaransa na kampuni ya Kizalendo ya Superdoll Tanzania Ltd.  wamezindua matairi yenye ubora na usalama kwa magari   aina ya Michelin  XM2 yenye  uwezo wa kuhimili barabara mbovu katika Afrika Mashariki na kati. Mkurugenzi mkuu wa Superdoll  Bw. Seif Ally Seif amesema matairi hayo yametengenezwa kwa utalamu wa kisasa ili kuzuia kupasuka yanapokanyaga kitu ambacho kina weza kusababbisha kupasuka. Amesema matairi hayo ya Michelin  XM2 yanapunguza gharama kwa watumiaji katika kuokoa fedha kwa vile yanadumu kwa muda mrefu na kuokoa matumizi ya mafuta.
 Mkurugenzi mkuu wa superdoll Bw Seif Ally (kulia)  akimsindikiza balozi wa ufaransa hapa nchini Mh. Marcel Escure ambaye alihudhuria uzinduzi wa kampuni ya Michelini Ufaransa katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam
Bwana Jamal Bayser akiwa na ofisa mwenzake wa kampuni ya Superdoll  na sanamu ya Michelin  

 Mkurugenzi mkuu wa superdoll bwana Seif Ally Seif akimuonyesha tairi hilo la xm2 Mnadhimu wa kikosi cha polisi usalama barabarani tanzania ASP Johansen Kahatano jinsi tairi hilo lilivyo imara. Katikati ni ofisa mahusiano wa kampuni ya superdoll tanzania bwana Ramoudh Ally.
Picha na habari na Chris Mfinanga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 07, 2012

    HONGERENI SUPERDOLL KWA BIDHAA ZENYE UBORA WA HALI YA JUU. MATAIRI YA MICHELIN NI IMARA NA MADHUBUTI.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...