Dr Engineer Shaban Kachua mwenye joho lenye rangi nyekundu na Bluu akiwa na waafrika wenzake wakati wa alipotunukiwa Shahada yake ya Udaktari wa falsafa Nchini Canada.
Hapa Dr Kachua akiwa amekaa mstari wa mbele kabisa na wahitimu wenzake.
Mama Mzazi wa Dr Kachua (mwenye blauzi nyeusi), akiwa na Mama mkwe wake, wote kwa pamoja walishiriki katika tukio la kihistoria la kutunukiwa Shahada ya PHD kwa mtoto wao nchini Canada.
Mrs Dr Shaban Kachua (Jemima) akiwa na furaha pamoja na watoto wao walishiriki katika shughuli ya kutunukiwa Mume wake shahada ya udaktari wa Falsafa (PHD).

Kwa sasa Dr Shaban Kachua anaishi Nchini Canada pamoja na familia yake. Sisi kama watanzania wenzake tunapenda kumpongeza sana kwa kuweza kuipeperusha vema Bendera yetu, tunapenda kumshauri pia, elimu yake hiyo aweze kuitumia pia kulisaidia Taifa lake la Tanzania hasa katika nyanja hiyo ya Sayansi, kwa kutambua zaidi tuna upungufu mkubwa wa wanasayansi katika Taifa letu.HONGERA SANA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 18, 2012

    hongereni Jemina na familia yako...

    nsubisi - dar!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 18, 2012

    Jemima hongereni sana


    beda - dar

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 18, 2012

    insikitisha kuona mtu anasoma miaka kadhaa kisha badala ya kulisaidia taifa lake anasaidia mataifa ya wengine-brain drain
    Kwanini sisi ni limbukeni wa nchi za watu, na kwanini tusijenge nchi zetu kwanza?

    Mtu akisikia ulaya au america basi anaweza kuuza nchi kwa dhaman ndogo mno. Tujenge nchi yetu kwanza, uwezo tunao, nguvu tunazo, nia hatuna.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 18, 2012

    Good Job buddy,on a different note, I will start to call my wife Mrs Dr Gangwe Bitozi, smirk.
    Dr Gangwe Bitozi.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 18, 2012

    Uncala sasa unatutia haibu what this "Dr engineer????" ukimwita Dr...., or engineer.... inatosha. Punguza uswahili.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 18, 2012

    nahitaji kusoma masters nje ya nchi ktk fani ya mhandisi ujenzi.nataka kusaidiwa kama kuna uwezekano wa kupata scholarship/sponsorshp...ijuvye hapa loptz@yahoo.co.uk

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 18, 2012

    Mkuu wa kazi SHABANI hongereni sana kaka tunajivunia kuwa na wewe mtu, nimefurahi sana kuona picha ya mama na GEMINA na watoto lol

    karibu Tanzania jimbo la Tanga mjini ni kama lipo wazi tuu uje tukupe lile jimbo MKUU

    PETER SHIRIMA

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 18, 2012

    Hongera sana Dr. Kachua. Salamu kwa familia pia.
    Bendera

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 18, 2012

    Hongera san Dr. Kachua na familia yako

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 18, 2012

    hongera sana Mkuu.duuh Wasomi wote wenye asili ya Tanzania kama wangekuwa na moyo wa kutoa ushauri au kufanya kazi za kujitolea wakati wa likizo zao Bongo,tungefika mbali sana.Bahati mbaya huo moyo haupo kwa watu wenye asili ya Tanzania au WaTanzania,ni wanchoweza ni kuilaumu Serikali usiku kucha.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 19, 2012

    Hongera sana Dr Eng. usisahau tu mambo ya slab pale foe!

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 19, 2012

    Ndugu mwandishi wa Fri May 18, 02:58:00 PM 2012. Punguza jazba, kila mtu anaamua kuishi kulinga na utasi wake. Huko kujenga taifa unakokusema ina maana mpaka leo hujajua hilo taifa lina wajenzi wake? Ndugu yangu kama wewe hujapata nasfasi ya kufika majuu basi waache waliofika waishi watakavyo. Tusipangiane maisha, just put your comment with regarding the guy success and not go further than that. I think it is clear and u'v understand. God bless you kwa maisha uliyochagua wish u success

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 19, 2012

    Baada ya shule kuisha, hapo ndipo Maumivu ya Kichwa huanza Pole Pole.
    Maana Recession ndo inazidi kushika hatamu kwa kasi ya ajabu.

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 19, 2012

    Kasheshe la Nigeria ni kuwa na wasomi mpaka ngazi ya Profesa lakini wako tu huko huko majuu wakibeba mabox.. We bwana rudi tu huku tujenge nyumbani kwetu hata kama utafundisha chekechea itasaidia maendeleo ya bongo

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 20, 2012

    Mdau wa Sat May 19, 06:14:00 PM 2012
    umezungumzia Nigeria, sasa huko wana wasomi kibao lakini hakuna ajira. Hivyo wenye PhD na hao Maproffesor ndiyo mainjinia wa kutengeneza Orginised Crimes na Fraud kwa kutumia internet. Tanzania ya leo njia ni hiyo hiyo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...