Jumuiya ya Watanzania Rome, inapenda kuwakaribisheni Watanzania wote nchini Italy kwenye sherehe ya Muungano wa Tanzania. Sherehe Itafanyika jumamos ya wiki hii tarehe 12 Mei 2012, kwenye Ukumbi wa Karispera Club 69, uliopo kwenye Mtaa wa Via Angelo Emo 69 mjini Rome, kuanzia saa kumi na moja jioni mpaka Lyamba! Kwa wale wote watakaotaka kushiriki mnaombwa muandike e-mail (watanzaniaroma.yahoo.it) au mpige simu 3479094800 ili muweze kupata maelezo zaidi ya namna ya kushiriki. Ticket zipo tayari na unaweza kuzipata kwa kumcontact Mwenyekiti, Mh. Leonce Uwandameno au Katibu (Nd. Andrew Chole Mhella) kwa contact za hapo juu.Tafadhali kwa wale wote watakao kuja mnaombwa msisahau ticket zenu.Kwa wale ambao watashindwa kupata ticket kabla ya siku ya sherehe mnaweza pia kuzipata mlangoni kwenye ukumbi.

NB: Itakumbukwa kuwa sherehe hii ilipaswa kufanyika tarehe 28 Aprili 2012, lakini kwa kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu tukaisogeza mbele wiki mbili.

Asanteni na Karibuni sana
Mungu Ibariki Tanzania. Mungu Ibariki Jumuiya ya Watanzania Roma.

Katibu,
Andrew Chole Mhella.
www.watanzania-roma.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...