TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua BIBI MWANAHAMISI OMARI KITOGO kuwa MSAIDIZI WA RAIS, HUDUMA ZA JAMII.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Y. Sefue leo, Jumanne, Mei 8, 2012, mjini Dar es Salaam inasema kuwa uteuzi huo umeanza Mei Mosi, mwaka huu, 2012.

Kabla ya uteuzi wake, Bibi Mwanahamisi Omari Kitogo alikuwa Mkadiriaji Ujenzi Msaidizi (Assistant Quantity Surveyor) katika Kampuni ya COWI, Tanzania.


Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
8 Mei, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 08, 2012

    Mkadiriaji ujenzi na huduma za jamii wapi na wapi jamani??????????

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 08, 2012

    Jamani huku utumishi (civil service) nasi wenye elimu, ujuzi na uwezo tuko twasubiri kupangiwa idara za kazi kuitumikia serikali yetu sehemu yetote serikarini. Huko sekta binafsi wawacheni huko huko kwani sisi tumeshatayarishwa kutumikia serikarini. alexbura dar

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 08, 2012

    Tatizolenu ni nini? Si na nyinyi muende huko.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 09, 2012

    From Assistant Quantity Surveyor to Assistant to the President, Social Services.

    mmh angemtupa kwenye ushauri wa ujenzi, usanifu na majengo.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 09, 2012

    Wewe mtumishi wa Serikali endelea kukaa ukisubiri Sitting Allowance uone kama utakumbukwa kwenye uteuzi wa aina yeyote.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...