Ubao ulivyokuwa unasomeka baada ya Yanga kupigwa na Simba mabao 5 kwa nunge katika Ligi Kuu ya Vodacom, kwenye Uwanja wa Taifa jijini  Dar es Salaam jioni ya leo.

Wachezaji wa Simba wakishagilia ubingwa baada ya kukabidhiwa kombe na Waziri Mteule wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangala

 Waziri Mteule wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangala (kushoto), akimkabidhi kombe la ubingwa wa Tanzania Bara baada ya mechi na Yanga kumalizika leo kwenye Uwanja wa Tgaifa, Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KAMANDA MWAIKENDA)

Wachezaji wakifurahia kombe

                                                 Simba wakishangilia ubingwa kiaina

Kocha wa Simba Milovan Circovic akiwa amebebwa na wachezaji
Wachezaji na viongozi wa Simba wakicheza mduara baada ya kuifunga Yanga mabao matano na kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara

 Wapenzi wa Simba wakishangilia ushindi wa mabao matano dhidi ya Yanga pamoja na ubingwa


                                                  Ni furaha kwa Simba kila mahala. 
Picha na Kamanda Richard Mwaikenda

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 06, 2012

    Mkono mmoja wenye vidole vinne watosha kuisambaratisha yanga na kuzidisha kizaazaa jangwani.

    Aminia Simba Taifa Kumbwa.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 06, 2012

    safi sana simba hongereni mnooo

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 06, 2012

    Kazi ya ukocha ni taaluma. Hivi miziro taaluma hii kaipatia wapi? Yanga ubishi kubishana na wenye taaluma zao. Matokeo yake ni kutunguliwa 5-0.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 07, 2012

    Tulisema kaa mbali na Simba.Hii ndo Simba ya Afrika na subirini makubwa zaidi.

    Hongera Simba,hongera viongozi,na hongera wanachama na wapenzi wote wa Smba.Umoja wenu umelipa.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 07, 2012

    Yanga hawakuwepo uwanjani nini?

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 07, 2012

    Hii ndio tofauti ya soka la kitabuni na soka la gazetini.
    Kabla ya mechi walisema sana ubingwa wameukosa lakini wataingia uwanjani na kulinda heshima yao. Na kweli! Umma umejua kiwango cha heshima yao kilipo.
    Hongera sana wekundu wa Msimbazi. Sherehekeeni leo lakini msibweteke. Mechi nzito za Afrika zinakuja.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 07, 2012

    Dah!! yaani hapa raha tupu...ubingwa na kumpiga Yanga bao 5-0...natamani ningekuwepo hapo uwanjani
    Mdau US.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 07, 2012

    Michuzi mbona nasikia mechi ilichezewa mezani ili kumkomoa Mwenyekiti baada baadhi ya wafadhili kumtaka aondoke na yeye kukataa. Kwa walioangalia mechi uvumi huu waweza kuwa kweli

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 07, 2012

    Ivi mwanume anapopigana na mwanamke akampiga hujisifia kweli?!! Ivi na nyie kwa akili zenu mnaona Yanga kuna timu ya kushindana na Simba akujipima kiwango kwa Simba mpaka Simba wakashangilia ushindi kwa kishindo!
    Simba ingepambana na wanume ndo itambe we unapambana na Yanga watoto wa kike unajitapa kama mjinga!

    Yanga ilikuwa zamani lakini sasa hakuna Yanga labda wajipange upya na vitu vipya na uongozi mpya.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 07, 2012

    duh huwezi amini yanga leo imetunguliwa 5-0 vichekesho ujue nn imedhihirisha ni kiasi gani kiwango chao kimekuwa. hongera sana simba mko juu kip it up

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 07, 2012

    Hizi bao 5-0 amefungwa Mjomba Muhidin Issa Michuzi kada wa Chama cha Mapinduzi, pamoja na Mchezaji NAMBA 1 wa Yanga Mhe. JK !

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 07, 2012

    Duhh gharika imetua Jangwani-2012 !

    Poleni Mhe. JK na Mjomba Michuzi kwa kipigo cha 5-0 !

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 07, 2012

    Kibelaaaah

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 07, 2012

    Kuna mdau mmoja juzi wakati azamu alipopigwa na Mtibwa akasema simaba wamepata ubingwa wa mezani a.k.a wa kusubiria matokeo ya wengine na alihitimisha hivi:
    ni kama majizi yamekurupushwa sehemu fulani halafu wakati yanafukuzwa yakaukuta mlago wako uko wazi wakati huo ww unaota kupata mipesa kisha unaamka unakuta hiyo mijizi iliyokurupushwa mahali imekuachia kapu la pesa.Sasa nataka kumsikia tena huyo mdau atuambie hiyo MIJIZI ilikuwa ni YANGA a.k.a kandambili!??

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...