Benki ya NMB jana imekabidhi zawadi za tani za saruji na mabati kwa washindi  wa droo ya kwanza ya promosheni ya ‘Jenga maisha yako na NMB’ iliyofanyika terehe 11 Julai 2012.



 Wateja wa Benki ya NMB, Victoria Maliseli, Ramadhan Mguya,Rehema Mohamed,Rose Mandera na Richard Makara wakifurahia kupata zawadi ya mabati 50 kila mmoja  na tani ya saruji kila mmoja(mabati wawili kushoto na tani ya saruji watatu kulia) pamoja na Mkuu wa idara yaMasoko na mawasiliano wa NMB Imani Kajula


Akizungumza katika hafla hiyo fupi iliyofanyika katika tawi la NMB Airport, Mkuu wa idara ya Masoko na Mawasiliano wa NMB Imani Kajula alisema kwamba, “NMB sasa inawezesha ndoto za watu kuwa kwelileo tunakabidhi tani za saruji na mabati.Hatimae ndoto za washindi sasa zimekuwa kweli na tunaamini promosheni hii sio tu kwamba itaongeza tabia ya kujiwekea akiba lakini itasaidia wateja walioshinda kufikia malengo waliojiwekea na pia kuboresha maisha yao”.

Mteja wa NMB Bi. Victoria Marisel akipokea mfano wa hundi yenye thamaniya mabati 50 kutoka kwa Meneja wa Huduma kwa Wateja wa NMB tawi la NMB Airport, Deogratius Mahawe.

NMB kwa kutambua kuwa watanzania wengi wanaweka akiba ili kutimiza malengo mbalimbali waliyojiwekea yakiwa  ni kujenga nyumba,kusomesha watoto na  kufikia malengo mengine  muhimu maishani mwao,  ilizindua promosheni inayowezesha wateja wa NMB Bonus Account an NMB Junior Account kuingia kwenye droo ya kushinda tani ya saruji,mabati ya kuwezeka,amana maradufu,ada za shule,fulana za NMB pamoja na mabegi ya shule kupitia promosheni ya Jenga maisha yako na NMB.

Katika droo ya kwanza washindi zaidi ya 167 walijishindia zawadi mbalimbali. Kushinda  ni rahisi sana, fungua akaunti au ongeza amana kwenye NMB Bonus Account au NMB Junior Account upatea riba ya kuvutia ambayo inaweza kuwa hadi asilimia 10 kutegemeana na kiwango cha amana ilichoweka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...