Na Geofrey Tengeneza –Yeosu Korea
Siku yaTaifa la Tanzania katika maonyesho ya Kimataifa ya Biashara ya Korea yanayofanyia katika jiji la Yeosu hapa Korea iliyofanyika tarehe 8/8/2012 iliweka historia na kuvutia maelfu ya wananchi wa Korea na watu mbalimbali kutoka mataifa mengine wanaoshiriki katika maonesho haya ikilinganishwa na siku mataifa mengi hususan kutoka barani Afrika.
Siku ya Tanzania ilianza kwa maandamano ya watanzania wanoshiriki maonesho hayo sambamba na wale wanoishi hapa mjini Yeosu yakiongozwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Dkt. Abdallah Kigoda yakianzia katika eneo maalumu la VIP ililo karibu na geti kuu la kuingilia katika viwanja vya maonesho hayo majira ya saa nne asubuhi yakipambwa kwa bendera ndogo zilizokuwa zikipungwa hewani  na watanzania hao wakiongozwa  ngoma ya Ngongoti iliyokuwa ikichezwa na kikundi cha ngoma kutoka Chuo cha Taifa cha Bagamoyo (TASUBA) huku maandamo hayo  yakishangiliwa na maelfu ya wananchi  wa Korea.
Hali ilikuwa ni tete zaidi katika ukumbi wa mikutano wa Maonesho hayo (Expo hall) ambapo maelfu ya wananchi wa Korea walianza kujikusanya mapema kabisa kuanzia saa 3.00 asubuhi kwa lengo ;la kuingia katika ukumbi ambao maandamano yangefikia  huku wakigombea maelfu ya bendera ndogo , DVDs na vipeperushi  mbalimbali vinavyoelezea utalii wa Tanzania vilivyokuwa vikitolewa na maafisa wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) , Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) na mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro (NCAA). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Ni Korea ipi DPRK (Korea ya Kaskazini) au South Korea (Republic of Korea)?

    Mdau
    Rufiji

    ReplyDelete
  2. na sisi wengine tunahitaji huku waje kuhamasisha watalii wa huku europe wanapenda sana hebu jaribuni tu kidogo muone mafanikio.

    ReplyDelete
  3. Jamani kumbe kuitangaza nchi ni rahisi sana kimataifa basi uwekwe mkakati kabambe..nahao ttb.tanapa.ncaa..kwa nchi zote za ugaibuni..hayo ndio mambo yanayo takiwa.. ni mm tajiri wa mawazo endelevu uk...amani kwa wadau wote.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...