Wazanzibari wanaoishi Canada ambao wanajumuika pamoja chini ya Jumuia yao ijulikanayo kama ZACADIA (Zanzibar-Canadian Diaspora Association) wameshitushwa na kusikitishwa na hali ya kiafya ya mtoto Nairat na dada yake pamoja na familia yao nzima kwa ujumla - kama walivyosoma huko nyuma kwenye ukumbi wa ZANZIBAR NI KWETU < http://zanzibarnikwetu.blogspot.ca/2012/08/please-help-this-kid-mtoto-nairat-seven.html>.
Kutokana na hali hio mbaya ya kiafya ya watoto, ZACADIA katika kusaidia matibabu ya Nairat na dada yake inatoa mchango wake wa TShs 750,014.04
Pesa hizo zimepelekwa Zanzibar leo tarehe 21 September, 2012 kutoka Canada kwa njia ya MONEYGRAM, kupitia  kwa Bi Salma Said ambae ni mdhamini wa hawa watoto kwa hivi sasa.
Kwa niaba ya Wana-Zacadia wote waishio Canada tunamtakia mtoto Nairat pamoja na dada yake shifaa ya haraka na kwa wakati huo huo tunaitakia Zanzibar kila mafanikio katika wakati huu mgumu wa kiuchumi kwa Ulimwengu mzima.
Kila la kheri.
Hassan Othman
Katibu / ZACADIA (Toronto, Canada).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...