MAREHEMU HERI YESAYA MASASI
Familia ya bwana na bibi
Yesaya Joseph Masasi wanapenda kumshukuru Mungu na pia kuwashukuru wote
waliofanyika faraja wakati wa kipindi kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao Heri Joseph tarehe 2/10/2009.
Shukrani za pekee ziwaendee
madaktari na wauguzi wa hospitali za Muhimbili na Tumaini, Wafanyakazi wa Tume
ya Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC), ndugu , jamaa namarafiki wa familia.
Unakumbukwa daima na baba na
mama, dada zako Vicky, Sara, Eva, Salome, watoto wako Erick na Sara, shemeji
zako Paulo, Godwill na Hariri, wapwa zako Melchior, Yesaya, Isaka, Jeni na Fathia,
ndugu na marafiki.
Tulikupenda sana lakini Mungu
amekupenda zaidi.
Kila siku tunakuombea kwa Mungu akupumzishe mahali pema.
Amen
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...