Tanzania 50 Plus Campaign ikishirikiana na wahanga wa saratani na marafiki wa kampeni itatembelea hospitali ya wagonjwa wa saratani katika hospitali ya Ocean Road. Ili kufanikisha zoezi hilo imeomba watu binafsi na makampuni mbali mbali na jamii kwa uumla kuchangia sabuni za kufulia, za kuogea, mafuta ya kujipaka (petroleum jelly), miswaki, dawa za miswaki, ndala, maji ya kunywa, juice mbalimbali na mtunda.

Katika kuitikia wito huo, Fatma Shabani Msungi, Mheshimiwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Kisutu, Kata ya Hananasif, Wilayani ya Kinondoni, alifika ofisini petu na kukabidhi boksi sita sabuni ya mbuni. Katika picha ni Bi. Msungi, akiambatana na Kikundi cha akinamama wa Warembo Forum,  akimkabidhi Dr. Emmanuel Kandusi, Mratibu wa Tanzania 50 Plus Campaign ambaye ndiye anayeratibu ziara hiyo kuwapa pole na kuwafariji wagonjwa wa saratani. Dr. Kandusi ni muhanga wa saratani ya tezi dume (prostate cancer).

Tanzania 50 Plus Campaign inamshukuru sana Mhe. Mwenyekiti kwa ukarimu wake na moyo wa upendo na huruma kwa wale wenye mahtaji.

Ukiwa na mchango wako wasiliana nasi:
Simu  0754 402033 au barua pepe: ekandusi@yahoo.com, chrptz@yahoo.com.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...