Mkuu wa benki kuu ya Zambia ndugu Mizinga Melu  amesema benki kuu ya Zambia (BoZ) imeandaa (workshop) ambayo itailezea kwa ufasaha benki inayofuta sheria za kiislam. Benki kuu ya Zambia ikiwa kama msimamizi mkuu itasimamia matayarisho hayo wakati timu ya wakaguzi (regulator) itakapokua tayari. ‘Wakati wowote unapoleta huduma mpya, ni muhimu kua sote tunazungumzia kitu ambacho tunafahamiana na tuanaweka malengo alisema mr Melu.
BoZ imenukuliwa ikisema ‘huduma za benki zinazaofuta sheria ya kiIslam zitawasaidia watu kupata mikopo isiyokua na riba kwa ajili ya kuzalisha mitaji yao’ na wakati huohuo inatoa changamoto kwa wajasirimali ambao wako tayari kuanzisha benki hizo nchini Zambaia.
Uchunguzi wa karibuni uliofanywa na benki kuu ya Zambia umeonyesha kwamba asilimia 80 ya mawasiliano yaliyofanywa yalionekana kuunga mkono huduma hizo na kuzikaribisha. Benki nyingi za biashara zinategemea kuanzisha huduma hiyo ikiwemo Standard Charted Bank na kuna soko kubwa la huduma hizo nchini Zambia na Africa kwa ujumla.
Kwa maelezo zaidi kuhusiana na benki zinazofuata sheria za kiislam wasiliana na http://ijuebankyakiislam.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Benki za Kiislam ni nzuri kwa wafanyabiashara.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...