AWAMU ya pili ya mradi wa Mazingira Bora kwa Elimu Bora, kwa kata ya Kipawa jijini Dar es Salaam inatarajiwa kuzinduliwa hapo kesho ambapo wadau mbalimbali wakiwemo Watu wa Marekani wamealikwa kushiriki kwenye uzinduzi huo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo diwani wa kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa, alisema lengo la mradi huo ni kuboresha Mazingira ya elimu ya Msingi na Sekondari kwenye kata yake.

Aidha Kaluwa alifafanua kuwa Uboreshaji huo wa mazingira ya Elimu unafanyika kwenye Shule saba za Msingi na Sekondary za kata hiyo kwa kuwapatia madawati, maji safi na salama, kujenga vyoo na madarasa pamoja na kuwapatia wanafunzi na walimu vifaa vya elimu.

Awamu ya kwanza ya Mradi huo ilizinduliwa Machi 17,2012 ambapo kwenye awamu hiyo kulifanyika kampeni za kuhamasisha wadau kuchangisha pesa na kufanikiwa kukusanya kiasi cha Tsh.155.5Million, ambazo zilitumika kwa kununua madawati 500 ya Shule ya Msingi, 480 Shule za Sekondari na viti 100 vya shule ya awali pamoja na kufanikiwa kuchimba kisima cha maji katika kila shule.
Awamu hii ya pili ya mradi itajihusisha zaidi kwenye ujenzi wa vyoo na madarasa.
Diwani wa Kata ya Kipawa jijini Dar es Salaam Bonna Kaluwa (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kuanza kwa awamu ya pili ya mradi wa Mazingira bora kwa elimu bora itakayozinduliwa rasmi hapo kesho kwenye kata hiyo, kulia ni Mtendaji wa serikali ya mtaa wa Kipawa Said Fundi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...