Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Ujenzi wa daraja la kisasa katika eneo la Mbutu,Wilayani Igunga leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua mradi wa Chujio la maji safi kwa mji wa Igunga sehemu za Bulenya ambapo wakazi zaidi ya asilimia 70 wa mji huo watapata maji safi.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia mashine ya kuchimbia mashimo ya nguzo za daraja kabla ya kwenda kukata utepe kwa kuashiria kuzindua ujenzi daraja la Mbutu,Wilayani Igunga leo.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanroads,Eng. Patrick Mfugale  (alieshika maiki) akumuonyesha Rais Kikwete ramani  ya Mradi wa Ujenzi wa daraja la kisasa katika eneo la Mbutu,Wilayani Igunga.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na kutoa ushauri kwa kundi la vijana 10 ambao baada ya kumaliza chuo kikuu wamejikusanya na kuunda kikundi cha ujasiriamali mjini Igunga wakijishugulisha na Kilimo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua sehemu ya vyanzo vya mradi mpya wa maji safi kwa mji wa Igunga sehemu za Bulenya ambapo wakazi asilimia 70 wa mji huo watapata maji safi
Wananchi wakivuka katika sehemu itayojengwa daraja la kisasa eneo la Mbutu,Igunga Mkoani Tabora ambao ujenzi wake umezinduliwa leo na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, hatua ambayo itatatua kabisa tatizo la miundombinu.PICHA NA IKULU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Ewe mwenyezi mungu mwingi wa rehema tusaidie haya mateso yapungue kama si kwisha kabisa, watu wanapata taabu sana ebu weka fikra ktk picha hii ya mwisho hapa chini, tafsiri ya haraka inayopatikana ni kwamba huo upande ambao watu wanaelekea pengine ndio wenye huduma muhimu za kijamii hivyo basi miaka nenda miaka rudi hayo ndio maisha yao hawa watanzania wenzetu wa huko.Mtoto mgongoni, begi kichwani na baiskeli juu.Kwakweli nakubaliana na wote wenye mapenzi mema na hii nchi hasa ktk wazo la kuendeleza mikoa husika kwa rasilimali zinazopatikana ktk mkoa huo kwa nia njema tu na si zote kuziamishia eneo moja ili kufanya watu kwabaki ktk maneo yao na kuyaendeleza, vinginevyo itakua kama ionekanavyo ktk picha hii hapo juu wote wanaovuka huo mto ni watu wazima kwa wazee yaani wale wasio weza kuondoka maeneo hao, yawezekana vijana wote wapo Dar. Hii pia itaepusha kukimbizana na mapolisi huku mjini.

    ReplyDelete
  2. miaka 50 baada ya uhuru tunatia aibu wakati baadhi ya viongozi wanamabilioni ya pesa uswis yaani nasikia uchungu sana,,,

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...