Mkurugenzi wa taasisi huru ya Superbrands Ukanda wa Afrika Mashariki Jawad Jaffer akimkabidhi Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group Hussein Dewji cheti cha tuzo ya ubora na thamani ya nembo kwa kampuni zinazotoa huduma bora kwa walaji katika hafla fupi iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group Hussein Dewji.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Raha Aashiq Sharrif (Kulia) akiwa Mwakilishi wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Raha Preetkamal Bansal ( wa pili kulia) wakati wa hafla fupi ya Superbrands kukabidhi vyeti kwa makampuni bora kwa mwaka 2013/14 iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa ITV na Radio One Bi. Joyce Mhaville ( wa pili kulia) aliyembatana na Mkuu wa Kitengo cha Masoko cha IPP Bi. Joyce Luhanga ( wa tatu kulia) wakati wa hafla ya utoaji wa cheti cha tuzo ya ubora na thamani ya nembo iliyoendeshwa na Taasisi ya Superbrands.
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group Hussein Dewji akibadilishana mawazo na mmoja wa wageni waalikwa katika hafla hiyo.

Taasisi huru ya Superbrands ambayo ni kubwa kuliko zote duniani, inayoratibu ubora na thamani ya nembo kwa kampuni zinazotoa huduma bora kwa walaji, leo imekabidhi vyeti vinavyotambuliwa kimataifa vya utambuzi wa ubora wa bidhaa kwa kampuni zilizofanya vizuri nchini Tanzania kwa mwaka 2013/2014.
Tuzo za Superbrands ni miongoni mwa tuzo zenye thamani kubwa na zinazoleta heshima ya pekee ndani ya kampuni.
Hii ni mara ya tatu kwa tuzo hizo kutolewa ndani ya Ukanda wa Afrika Mashariki tangu kuanzishwa kwake yapata miaka mine iliyopita.
Uamuzi na hatimaye utoaji wa tuzo husika unatoka baraza huru la wataalamu waliobobea katika masuala ya biashara, lakini lengo hasa likiwa ni ni kustawisha na kuhamasisha ari katika utoaji huduma zinazo zingatia ubora.
MeTL imekuwa moja wapo kati ya Makampuni yaliyopokea vyeti vya tuzo hizo zilizofanyika kwa mara ya tatu hapa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Sawa tunaamini haki imetendeka ktk utoa Tuzo.

    Lakini ule upuku puku wa Makampuni yetu akina Maganga na Mukalamaka ya Usindikaji na Huduma za Ulaji kama,

    *Haya twende Producers T. Ltd.,
    *Bora nile Holdings Co.T Ltd.,
    *Kheri nimepata Co.T

    Yako wapi hapo?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...