Mrs. Leticia Daudi Lusala

Mungu wetu ni Mwema, ametuliza mioyo yetu katika mwaka huu mzima wa ukiwa na majonzi mengi kwa kumkosa mpendwa wetu Leticia. Ndio maana tunajumuika tarehe 8 na ( ili kushukuru mungu na kumwomba amweke mahali pema peponi amina.

Familia ya Mr. Lusala inapenda kuwakaribisha katika misa ya kutimia kwa mwaka mmoja tokea tulivyompoteza mama yetu mpendwa marehemu Leticia Lusala,itakayofanyika kwa mkesha siku ya ijumaa hii tarehe 8, na siku ya jumamosi tarehe 9/02/2013 kutakuwa na misa katika kanisa la Sinza Katoliki saa 3 asubuhi,halafu safari ya kwenda makaburini kinondoni kwa sala fupi, tunaomba wote tujumuike kumsalia na kumsindikiza mama yetu mpendwa.

Kwa habari zaidi wasiliana na Seraphin 0786303038 na Edward 0754091883

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...