Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Bi. Mwanamvua Ngocho, akizungumuza na wageni waalikwa, abiria waliosafiri na ndege la shirika hilo, pamoja na maofisa wa uwanja wa ndege la Mtwara (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa safari za ndege za Shirila la Ndege la Tanzania (ATCL) mkoani Mtwara , mara tu baada ya kutua ndege hiyo uwanjani hapo mwishoni mwa wiki.
 Meya wa Mtwara Mikindani, Selemani Mtalika Shilingi ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa safari za ndege za Shirila la Ndege la Tanzania (ATCL) mkoani Mtwara, akizungumuza na wageni waalikwa, abiria waliosafiri na ndege la shirika hilo, pamoja na maofisa wa uwanja wa ndege la Mtwara (hawapo pichani) mara tu baada ya kutua ndege hiyo uwanjani hapo mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Bi. Mwanamvua Ngocho na kulia ni Meneja Rasilimali watu na Utawala, Bi. Halima Nabalang’anya.  
Baadhi ya abiria waliopanda dege ya Shirika la ndege la Tanzania (ATCL), wakitembea kuelekea katika chumba cha kupumzikia abirai, wakati wa uzinduzi wa safari za ndege za shirila hilo mkoani Mtwara iliyofanyika mwishoni mwa wiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Hongereni sana ATCL. Great job.Im very proud of you. Mrs Ngocho, you look great my sister..Madia jr

    ReplyDelete
  2. Hongereni sana lakini kuna angalizo moja.Jitahidini kuongeza ndege hata ya kukodi kwani chochote kikitokea kwa ndege hii ndo tena miezi mitatu mnakaa bila usafiri.Nchi nzima na ma resources yote hatushindwi kununua hata ndege used

    ReplyDelete
  3. hongera atc na wakazi wa mtwara naomba atc mtufikirie nasisi wa songea jamani basi linachokesha.

    ReplyDelete
  4. Hakuna sababu ya kuendelea kukodi Madege!

    Kwa nini tusinunue mpya?

    Hiv jamani naomba niulize, nchi kama Rwanda ambayo masikini weee Uchumi wake wanategemea kilimo cha majani ya Chai, Kilimo cha Mauwa na Utalii wa Manyani kwenye Milima yao ya Kusini ya Mt.Ruhengeri WAMEMUDU KUNUNUA NDEGE TENA MPYA (BRAND NEW) BOEING 747 KADHAA HIVI, JE SISI AMBAO NDIO KWANZA TUNA UPUKU PUKU WA MIMALI TUNASHINDWA NINI?

    ReplyDelete
  5. hao waajiriwa kwanza hawana uweza wa kuipeleka shirika mbele, am here to witness

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...