Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Mwinyihaji Makame Mwadini,(kulia)  akimkabidhi zawadi ya Kasha  Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman  Yussuf bin Alawi bin Abdullah,akiwa kiongozi wa ujumbe wa Serikali ya Watu wa Oman,baada ya  hafla ya chakula maalum,kilichoandaliwa kwa ujumbe huo,katika Hoteli ya Serena Mjini Zanzibar
 Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman  Yussuf bin Alawi bin Abdullah,akitoa hutuba fupi ya  shukururani zake kwa kuandaliwa chakula  maalum,akiwa na ujumbe wake katika Hoteli ya Serena Mjini Zanzibar 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Mwinyihaji Makame Mwadini,(kushoto) alipokuwa akitoa hutuba fupi ya kuwashukuru wageni  wa ujumbe wa Serikali ya Watu wa Oman,ulioongozwa na  Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman  Yussuf bin Alawi bin Abdullah,(kulia) baada ya kushiriki katika  hafla ya chakula maalum,katika Hoteli ya Serena Mjini Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. 'Chakula cha usiku' kweli Waarabu watakubaliana nacho?

    Hivi sasa Lugha yetu ya Kiswahili imepanuka sana, kwa haraka haraka unaposikia neno 'chakula cha usiku' unakuwa umeshafika mbali zaidi ya maana yenyewe ilivyo.

    Nadhani Wageni wakielekezwa Kiswahili kwa undani zaidi watapendekeza wale cha mchana!!!

    ReplyDelete
  2. Bwana Yusuf bin Alawi waziri wa mambo ya nchi za nje wa Oman ana miaka 30 au zaidi katika wizara hio. Mkongwe wa mambo ya kisiasa yake ni mambo kimya kimya kunapotokea mgogoro wowote duniani. Ni mmoja wa wana siasa wachache ambao siasa yake ni kutoingilia mambo ya nchi zingine katika mambo yake ya ndani. Tunakumbuka vita vya ghuba Oman iliomba Iraq na Kuwait wakae meza moja ili kuepuka balaa la kuingiliwa na mataifa makubwa nadhani mwisho wake mnaujua ni nchi zote mbili kuteketea watu na mali!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...