Balozi Ignace Gata Mavita wa Lufuta, Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika Umoja wa Mataifa, akilizugumza Baraza Kuu la Usalama la UM, mara baada ya Katibu Mkuu, Ban Ki Moon kuwasilisha mbele ya Baraza hiyo Taarifa yake kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Maziwa Makuu. Katika maelezo yake, Ban Ki Moon amelitaka Baraza kuridhia haraka iwezekanavyo upelekaji wa Brigedi Maalum (intervention Brigade) katika DRC. Brigedi hiyo itakuwa na dhamana pana ikiwamo ya kukabiliana na makundi ya wanamgambo wenye silaha ndani ya DRC na wanaotoka nje ya nchi hiyo na hususani katika eneo la Mashariki ya nchi hiyo.
Na Mwandishi Maalum
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon,
amelitaka Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa kuidhinisha haraka iwezekanavyo
upelekaji wa Brigedi maalum ya Kijeshi
katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ( DRC) ili iweze kukabiliana na tishio la usalama na
amani katika eneo hilo.
Mkuu
huyo wa UM ametoa wito huo siku ya jumanne, wakati alipowasilisha mbele ya
Baraza hilo , taarifa yake kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na eneo la
Maziwa Makuu.
Akilizungumza Baraza hilo, Katibu Mkuu ameeleza bayana kwamba hali katika DRC ni tete na inahitaji maamuzi ya haraka.
Brigedi
hiyo maalum ijulikanayo kama Intervention Brigade itakuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa, ama kushirikiana au kutoshirikiana na Jeshi la kitaifa la DRC, dhidi ya makundi mbalimbali ya wanamgambo wenye
silaha ambao wamekuwa wakihatarisha hali ya amani na
usalama katika eneo la Mashariki ya DRC.
Katika taarifa yake kwa Baraza la Usalama la UM, Ban Ki Moon
amependekeza kwamba Brigedi hiyo maalum
itakuwa chini ya Misheni ya
Kutuliza Amani ya Umoja wa Mataifa
katika DRC maarufu kama MONUSCO kwa
mwaka mmoja
“
Brigedi hii maalum na ambayo chimbuko lake
linatokana na maamuzi ya Kikanda
inalenga katika kukabiliana na
tishio dhidi ya hali ya utulivu na usalama na itawajibika katika kujibu
mapigo kupitia MONUSCO.
Katibu
Mkuu amebainisha zaidi kwa kulieleza
Baraza Kuu la Usalama kwamba, Brigedi hiyo ( Intervention Brigade) itakuwa na
dhamana ya kukabiliana dhidi ya
kupanuka kwa makundi yenye silaha ya
Kikongo na yale ya kigeni, kupunguza nguvu za makundi hayo pamoja na
kupokonya silaha. Na kwamba upelekwaji
wa Brigedi hicho utaongeza nguvu.
Kuanzishwa
kwa Brigedi hiyo maalum kunalenga kuunga
mkono Mpango mpya wa amani, ulinzi na ushirikiano kuhusu DRC na eneo la maziwa
Makuu, mpango ambao ulitiwa saini na viongozi kadhaa wa Afrika Februari 24, 2013 Addis Ababa, Ethiopia.
Aidha
katika upelekaji wa Brigedi hiyo maalum
Umoja wa Mataifa utakuwa mdhamini ukishirikiana na Umoja wa
Arika, Jumuiya ya Mendeleo ya
Nchi za Kusini mwa Afrika ( SADC) na
Mkutano wa Kimataifa wa Nchi za Maziwa Makuu ( ICGLR).
Baada
ya kuwasilisha taarifa yake, akitekeleza
agizo la Baraza Kuu lililomtaka kuwasilisha taarifa kuhusu
hali ya DRC na hatua ambazo anachukuwa. Hatua inayofuata ni kwa Mkuu huyo wa UM
kumteua Mwakilishi wake Maalum, ambaye
kwa kushirikiana na wadau wengine, anatarajiwa kuunga mkono utekelezaji wa makubaliano yaliofikiwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...