Jengo la kituo cha mafuta cha Woco oil kilichokamatwa kwa wizi wa umeme





Mmiliki wa White Parrot hotel na kituo cha mafuta cha Woco Oil vyote vikiwa Korogwe mkoani Tanga anatuhumiwa kutumia umeme wa wizi kwa kuharibu mita nne zilizo katika majengo yake ya hotel na kituo cha mafuta. 
 Mmiliki huyo anasemekana ndie mmiliki wa kituo cha mafuta cha Woco Oil kilichopo Kongowe, Mkoa wa Pwani, ambacho miezi michache iliyopita alikutwa pia anatumia umeme usiopimwa. Na katika hali isiyotarajiwa imefahamika Woco Oil ya Korogwe ndio wanaoliuzia Shirika umeme Tanesco mafuta kwa wilaya ya Korogwe. 

Mhandisi wa Tanesco Francis Maze aliyeongoza operesheni hiyo amesema inasikitisha kuona kampuni inayofnya biashara na Tanesko kuwa ni mmoja ya wahujumu wa shirika. Mauzauza hayo yalikutwa pia katika Hoteli ya Hale, na wamiliki wa hoteli zote hizo hawakuweza kupatikana kwa madai wako nje ya Tanga. Ila bado wanatafutwa

Hale view hotel,imebainika inatumiwa umeme wa wizi baada ya kikosi maalumu tooka makao makuu ya Tanesco ikiongozwa na mhandisi Francis Maze kufanya ukaguzi wa mita .


Sehemu ya jengo la Hale view hotel

Mita zilizoharibiwa
Jengo la hotel ya White Parrot na camp site iliyokamatwa kwa wizi wa umeme, hotel hii iansemekana  mmiliki  wake ni mmoja na kituo cha mafuta cha Woco oil Korogwe,pamoja na cha Kibaha ambacho pia kilikamatwa.

Mita iliyoharibiwa Hale View hotel



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Huyu ni Mzoefu! kama mnataka watu wote waache WIZI huu BASI nawashauri huyu jamaa ANYONGWE!

    ReplyDelete
  2. huyu bila ya shaka atakuwa mtu wa .................. Hao wizi kwao ni mila

    ReplyDelete
  3. wafanyakazi wa TANESCO wanahusika kuanzia wahasibu , mameneja wa mikoa hadi vishoka, msijifanye hamjui na wala hilo sio jipya.

    ReplyDelete
  4. viongozi wenyewe wezi ije kuwa watumishi wa chini waache waibe tu hiyo nchi kila mtu ale kwa uwezo wa mbinu zake

    ReplyDelete
  5. Bei ya umeme ni kubwa mno.Mimi namtafuta fundi anikorofishie mita kwani naona gharama za umeme ni kubwa mno wakati raasilimali ya kuzalisha umeme ni bure, Mungu aliumba mito ya kutiririsha maji yanayozalisha umeme. Hata hiyo gesini mali ya Mungu, msituzingue.BEI YA UMEME NI KUBWA MNO.

    ReplyDelete
  6. Mdau wa Wed Mar 06, 07:08:00 am 2013: Mbona hunatisha? Mtu anyongwe kwa kuiba umeme? Hiyo kali.
    Nakubalina na Mdau wa Wed Mar 06, 11:24:00 am 2013
    Kweli Bongo watu wengi ni waizi wa aina fulani na wanokamatwa ni hao wa chini. Yaani kila kitu Bongo nao ujanja fulani. Mie namshangaa jamaa anayesema tuandamane kwenda ubalozi wa Uingereza kumpinga yule mama Mzungu, kwa vile kasema Bongo rushwa ni nje' nje' Ni Ukweli. Tukianza na Uongozi wa Taifa wenyewe una utata na asiyejua chama tawala uchaguzi ulinuka rushwa? Rushwa kwa trafiki, hospitali, Uwanja wa ndege, Mahakamani, mashuleni, michezoni. Ni aibu. Nadhani imekuwa kawaida sasa, yaani watu mpaka hatuoni rushwa ni wizi.

    ReplyDelete
  7. Mbona wamekimbilia mikoani?
    Wamulike hapo Dar,mtakayoyaona mtalia,

    Viwanda,magodown,majumba yoote makubwa ya biashara,nk wizi kwa kwenda mbele.

    Kuna mtandao mkubwa sana wa wizi.Bila mikakati imara tanesco haina jinsi lazima ife.

    Naamini tanesco wakijipanga watagundua "Lakuongezwa ktk maajabu saba ya dunia"

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...