Hapa ni katika makutano ya barabara za Jamhuri na Azikiwe Avenue katikati ya jiji la Dar es salaam. Baada ya wajuaji kupora mfuniko wa chemba ya maji taka limebaki bonge la shimo katikati ya barabara na wasamaria wema wameweka jiwe la msingi ili kukutahadharisha na mradi huo ambao kila baada ya muda unatema maji taka yanayonukia si mchezo. Hii ni wiki ya nne sasa shimo hilo na mengine kadhaa pembeni yanakenua tu....
Home
Unlabelled
yale yaleeeee
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Hivi hao wanaopokea mifuniko hiyo na kuinunua, wana akili sawa? Ni sawa na mtu anayenunua cheni, saa, nk nk vya wizi. Ningekuwa serikali ningefunga viwanda vya vyuma chakavu vyote wapate adabu. This is vandalism. Na inaendelea for decades, serikali imelala usingizi.
ReplyDeleteNa mimi naungana na mdau wa kwanza hapo juu,naongeza kwa kuvilaumu vyombo vyetu vya dola(polisi na usalama wa Taifa),ni wajibu wao kumtafuta na kumkamata huyu anayenunua mifuniko na vyuma vingine chakavu.Atafutwe akamatwe huyu 'mnunuzi' wa hii mifuniko na afunguliwe makosa ya uhaini.Nilisoma Gazeti la Daily News majuzi, eti TBS wanakamata wanaouza Nondo FAKE!Kamata viwanda vinavyotengeneza nondo feki fungia.Finish
ReplyDeleteWee vipi ufunge viwanda, jaribu uone hizi biashara za watu tena wana nguvu mfano hakuna. Leta mdomo mdomo wako likikutokea la kukutokea usije ukalaumu mtu buree.
ReplyDeletemimi naona tujaribu kutafuta teknologia ya kutengeneza hivi vifunkio kwa "material" tofauti badala ya chuma.Hivyo basi hao wezi hatakuwa na sababu ya kuvichukua.
ReplyDelete