Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania, Bw. Koenraad Adam akizindua programu ya utawala bora na ujasiriamali kupitia tafiti, elimu na teknolojia iliyofanyika Chuo Kikuu Mzumbe jana. Wengine ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Taaluma, prof. Josephat Itika na baadhi ya washiriki katika hafla hiyo.
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Taaluma, Prof. Josephat Itika (katikati) akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa programu za utawala bora na ujasiriamali kupitia tafiti, elimu na teknolojia iliyofanyika chuoni hapo jana. Wengine katika picha ni Prof. Auleria Kamuzora (wa kwanza kushoto), Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Morogoro, Bw.Noel Kazimoto (wa pili kushoto) na Balozi wa Ubelgiji Nchini, Bw. Koenraad Adam.
Balozi wa Ubelgiji nchini, Bw. Koenraad Adam akisisitiza jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa programu za utawala bora na ujasiriamali kupitia tafiti, elimu na teknolojia Chuo Kikuu Mzumbe jana. Wengine ni Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Morogoro, Bw. Noel Kazimoto (kushoto), Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Taaluma, Prof Josephat Itika na Prof. Auleria Kamuzora (kulia).
hicho kibao kinatoa hisia ya wahusika wa Mzumbe wako serious kiasi gani na huo mradi
ReplyDelete