Mhe.Job Ndugai,Mbunge wa Kongwa na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania akiongoza Mkutano wa Kamati ya Mazingira na Jamii cha Umoja wa Mabunge ya Nchi za Afrika,Caribbean na Pacific.Naibu Spika anashikilia wadhifa huo kwa kipindi cha miaka mitatu baada ya kuchaguliwa na wajumbe hao mwaka jana.Umoja huo una jumla ya nchi wanachama 79.Mikutano ya Umoja huo hufanyika mara nne kwa mwaka ambapo nchi wanachama huandaa katika nchi zao mikutabo miwili na pia miwili hufanyika Brussels ili kuwawezesha kukutana na wabunge wenzao wa Jumuiya ya Ulaya.Mkutano huo aliouongoza Mhe Naibu Spika hicho pamoja na mambo mengine ulifanyika ili kuweka msimamo wa pamoja kabla ya kukutana na wabunge toka Jumuiya ya Ulaya hapo kesho. Wengine pichani ni Nd.Kasule wa Sekretarieti ya ACP(kushoto),Makamu Mwenyekiti toka Chad,Mhe.Dr Mary Mwanjelwa wa Viti Maalum Mbeya na nyuma yake ni Mhe.Mussa Azzan Zungu,Mbunge wa Ilala.Picha na Saidi Yakubu wa Ofisi ya Bunge.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...