Na Woinde Shizza

Wakazi wa eneo la mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro wakipokea chakula cha msaada kutoka kwa uongozi wa Ngorongoro Conservation Are Authority (NCAA) ikiwa ni agizo kutoka kwa waziri mkuu mizengo pinda.

Tani 7000 zimegawiwa kwa familia 20,000 za jamii ya wamasai wanaoishi katika hifadhi hiyo. Idadi ya watu ndani ya NCAA kwa sasa ni zaidi ya 87,000 na wote wakiwa na mahitaji makubwa ya chakula kwani hawaruhusiwi kulima ndani ya eneo la NCAA.

Hivi karibuni wamasai hao wamejukuta wakikumbwa na baa la njaa baada ya ukame ulioathirini eneo lao kwa miaka mitatu mfululizo kuteketeza mifigo ambayo hasa ndiyo tegemeo lao la maisha.

Ugawaji wa chakula umeanza katika kata ya Olbalbal na utaendelea kwenye maeneo mengine huku NCAA ikijiandaa kununua tani zingine 29,000 za mahindi kutoka wilayani Karatu kwa ajili ya kuongeza mgawo huo wa chakula.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...