Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na watumishi wa Idara ya Uhamiaji Makao Makuu pamoja na wawakilishi wa idara hiyo Mkoa wa Dar es Salaam (hawapo pichani) kuhusu masuala mbalimbali ya utendaji kazi wa idara hiyo. Kulia ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil pamoja na Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylvester Ambokile Mwakinyule. Dk Nchimbi aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa uadilifu. Mkutano huo ulifanyika katika ofisi za Uhamiaji Makao Makuu, jijini Dar es Salaam leo.
 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na watumishi wa Idara ya Uhamiaji Makao Makuu pamoja na wawakilishi wa idara hiyo Mkoa wa Dar es Salaam. Dk Nchimbi alifanya ziara ya siku moja katika Ofisi za Makao Makuu ya Idara hiyo, Kurasini jijini Dar es Salaam leo kwa lengo la kuzungumza na watumishi hao masuala mbalimbali ya utendaji kazi..
 
  1. Kamishna wa Pasipoti na Uraia, wa Idara ya Uhamiaji, Victoria Lembeli (kushoto) akimuuliza swali Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wa pili kutoka kulia) kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo ya idara hiyo. Watumishi mbalimbali waliuliza maswali pamoja na kutoa maoni yao katika mkutano huo uliofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya idara hiyo, Kurasini jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima. Kushoto (Meza Kuu) ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil pamoja na Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylvester Ambokile Mwakinyule. (Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Na vipi kuhusu KIMBUNGA? Mm binafsi sipo HAPPY na utekelezaji wa agizo la RAIS wetu,yani mm sielewi kabisa au hamkumuelewa nn alichokwambieni? Coz DAR ndio yenye wahamiaji wengi zaidi zile siku 14 alizotoa Muheshimiwa RAIS msichukulie kwenye hiyo MIKOA pekee bali ni NCHI NZIMA,kwa mtazamo wangu NYIE ndio mlio sababisha haya MATATIZO YOTE kwakua hamko MAKINI na KAZI ZENU,mpaka RAIS amekwambieni mko ZAIFU SN na hili halina kificho kwenu lipo wazi kabisa kwenu tena mshukulu Hajaivunja hii wizara,sasa bc tunataka kuona MSAKO NCHI NZIMA,na sehemu za kuanzia hizo hapo maana kila kitu nyinyi mnasubili mpaka muambiwe,MITAANI,MAHOTELINI,VIWANDANI,KWENYE MIGODI ya DHAHABU,KWENYE MASHULE,KWENYE MAMBUGA YA WANYAMA,na KWENYE WIZARA ZOTE,,ndugu zangu naomba nanyie mnisaidie sehemu ambayo labda mnaona sikuitaja,mm naitwa mdudu KAKAKUONA napatikana huku Uingereza,haya wadau kazi kwenu,na nawapendeni woote huko Nyumbani

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...