Kesi za unyanyasaji dhidi ya wanawake zinazidi kuwa nyingi. Wanawake
wameendela kuumizwa na ubabe wa waume zao. Hivi karibuni, katika kijiji cha
Kizanda wilayani Lushoto mkoa wa Tanga, mwanamke mmoja aliyejulikana kwa
jina la Bi. Rahima alifariki dunia baada ya kupigwa na mumewe mateke ya
tumboni angali mja mzito.
Taarifa za awali kutolewa zinasema kuwa mwanamke huyo alifariki kutokana na
homa, lakini ndugu wa marehemu wamedai kuwa kifo cha ndugu yao kimetokana
na kipigo. Bi Rahima ambaye alikuwa ni mja mzito, alifariki mwezi wa saba
mwaka huu.
Taarifa za awali ambazo zilifikia Wanawake Live na Super Woman Joyce Kiria
kufuatilia zilionekana kupita EATV usiku wa jana, na pia unaweza kufuatilia
kwenye YouTube kupitia linki hii hapa chini ili ufahamu kile wanasheria
wamekizungumza katika kutafuta haki kufuatia suala hili ambalo hata
viongozi wa kijiji hicho wameshindwa kulitatua.
vipindi kama hivi ni muhimu sana kuliko hata usanii wanaokalia wabunge kwani vinaendana na jamii halisi.You are super woman Big up Joyce.keep going tutafika
ReplyDeleteTatizo la serkali Linachagua viongozi mrradi haizingatii, umuhimu wa jukumu analotakiwa kuwa nalo kiongozi hasa mashina kata kijiji mapaka ngazi za juu za uongozi. Mtu anachukuawa uongozi mradi kama pana masilahi apate mradi wake kwa kweli hatutafika kwa mpango kama huu serikali lazima iwe makini sana
ReplyDeleteIvi huyu ni balozi anamuongoza nani huko Tanzania??????Mtu amekimbilia kwako baada ya kupigwa na mumewe,wewe kama kiongozi hatua uliyochukua ni kumwambia lala hapa!Ama kweli tuna safari ndefu sana.Amenikera huyu mwanamke,Napata picha ya hiyo jamii anayoiongoza hapa kijijini kwake.
ReplyDelete