Uongozi wa Tawi la CCM - Moscow chini ya mwenyekiti wake Dr. Alfred Kamuzora unatoa shukrani zake za dhati kwa Naibu Waziri wa uchukuzi  Dr. Charles Tizeba kwa mchango wake wa hali na mali kwa Tawi, tunamshukuru sana kwani mchango wake umeongeza imani ya wanachama na kujua kuwa viongozi wa chama wako pamoja nao.

Katika kikao kifupi na viongozi wa Tawi mwenyekiti amemuelezea naibu waziri Dr. Tizeba kuwa ni kiongozi mahili kwani ni kiongozi ambaye mahali popote yupo tayari kukitetea na kukilinda chama kwa kila hali. Huu ni ujasiri ambao ametuachia sisi kama viongozi wa Tawi kusimamia itikadi na sera za chama mahali popote na wakati wowote.

Dr. Kamuzora alisema kuwa Dr. Charles Tizeba ambae ni Naibu Waziri wa Uchukuzi ni mfano wa kiongozi wa kuigwa kwani ni kiongozi asiyependa urasimu kwani ni muwazi na mtendaji na ambae anakubali kusikiliza na kutoa ushauri na uamuzi pale ambapo uamuzi huo unatakiwa kutolewa na yale yakufanyia kazi basi anayatolea maelezo. 

Hii ilibainishwa katika mkutano ambao Naibu Waziri aliufanya alipokutana na watanzania pamoja na maofisa wa ubalozi wa watanzania jijini Moscow nchini Urusi.

Wakati huo huo Dr. Kamuzora amewataka viongozi wa Tawi kuiga mifano ya viongozi kama hawa wenye ujasili na wasiopenda urasimu kama ilivyoonekana kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi Dr. Charles Tizeba.

IMETOLEWA NA UONGOZI, TAWI LA CCM MOSCOW

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tawi la Republican kufunguliwa next month hapa Uvinza. Please board the train to Kigoma and drop at Uvinza Railway Station. Chipukizi watakuwa hapo kuwapokea. Tunashukuru wananchi wote kwa michango yenu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...