Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania London unawakaribisha Watanzania wote watakaoweza kupata fursa kuja kuzungumza na Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Christopher Chiza na Wawakilishi kutoka SAGCOT hapo Ubalozini siku ya Jumatano (tarehe 23 Octoba 2013) kuanzia saa Kumi na Moja jioni (17:00).

Mheshimiwa Waziri anatarajiwa kuzungumzia masuala mbalimbali ya Kilimo, fursa zilizomo katika kilimo na ushirikishwaji wa Diaspora katika uwekezaji katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya nchi. Aidha Mhe. Christopher Chiza anatarajiwa kujibu maswali mbalimbali kutoka kwa wananchi watakaohudhuria mkutano huo.

IMETOLEWA NA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA, LONDON

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. venue wapi au ubalozini...please niko interested

    ReplyDelete
  2. kilimo kwanza...sisi tunasemaa dual citizenship kwanzaaaa....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...