Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Uingereza, Prince Charles ambaye pia ni Mtoto wa Malkia wa nchi hiyo, Malkia Elizabeth II ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua zake za dhati za kulinda wanyamapori na kupambana na ujagili dhidi ya tembo na faru.
Aidha, Prince Charles amesema kuwa yuko tayari kuunga mkono juhudi hizo za Tanzania kwa kushirikiana na mtoto wake, Prince William ambaye amechagua shughuli za kulinda wanyamapori na kupambana na ujangili duniani kama moja ya shughuli zake kuu.
Moja ya hatua ambazo Prince Charles ameamua kuchukua ni kukabiliana na soko la bidhaa kuu za ujangili duniani, na hasa meno ya tembo na faru, na kufanya kampeni kubwa duniani dhidi ya biashara hiyo haramu.
Prince Charles ametoa pongezi hizo na msimamo wake wa kuunga mkono jitihada za Tanzania wakati alipokutana kwa mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. Viongozi hao wamekutana kwenye Jumba la Tintagel mjini Colombo, Sri Lanka, ambako amefikia wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola (CHOGM) ambao Prince Charles ameufungua rasmi asubuhi ya leo, Ijumaa, Novemba 15, 2013, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mahinda Rajapaksa.
Rais Kikwete naye yuko Sri Lanka kuhudhuria Mkutano huo. Wakati wa mazungumzo hayo, Rais Kikwete ametumia muda mrefu kumwelezea Prince Charles kuhusu hatua ambazo zimekuwa zinachukuliwa na Serikali yake kupambana na ujagili dhidi ya tembo na faru ikiwamo Operesheni Maalum – Operesheni Tokomeza -ambayo ilifanyika hivi karibuni kuwasaka na kukabiliana na wafanya biashara haramu ya meno ya tembo.
Rais Kikwete amemwambia Prince Charles kuwa pamoja na kuchunguza malalamiko yaliyotolewa na makundi mbali mbali ya watu kuhusu operesheni hiyo ya kwanza, bado operesheni hiyo itaendelea kwa sababu ni muhimu kulinda wanyamapori dhidi ya majangili. “Imefika mahali ambako tunahitaji kuchukua hatua kali.
Wakati wa Uhuru wetu kulikuwepo na tembo kiasi cha 350,000 lakini ilipofika mwaka 1989 idadi hiyo ilikuwa imepungua na kubakia 55,000. Hata hivyo, baada ya operesheni maalum na kubwa, idadi hiyo ilikuwa imeongezeka hadi kufikia 110,000 kabla ya kuanza wimbi jipya la ujangili mwaka 2010. Operesheni lazima iendelee,” Rais Kikwete amemwambia Prince Charles.
“Tusaidie kufunga na kuvuruga hili soko la bidhaa za wanyampori. Operesheni ya sasa imethibitisha kuwa mtandao wa uwindaji haramu na biashara haramu ya meno ya tembo na faru ni mkubwa na watu wengi wanahusika, lakini kinachovuruga zaidi ni kwamba lipo soko la uhakika la meno ya tembo.”
Prince Charles amemweleza Rais Kikwete kuhusu hatua ambazo anakusudia kuzichukua kukabiliana na hali hiyo, ikiwa ni pamoja na kuandaa mkutano mkubwa wa wakuu wa nchi na Serikali Februari 13, mwakani na kufanya mkutano mwingine mkubwa na vyombo vya habari kutoka pote duniani mwakani.
“Nakusudia pia kutumia wasanii nyota mbali mbali duniani kuendesha kampeni ya kuielimisha dunia kuhusu athari za biashara hiyo haramu kwa sababu asilimia kubwa ya mapato ya ujangili inasaidia kugharimia vikundi vya kigaidi duniani.”
Aidha, Prince Charles amesema kuwa yuko tayari kuunga mkono juhudi hizo za Tanzania kwa kushirikiana na mtoto wake, Prince William ambaye amechagua shughuli za kulinda wanyamapori na kupambana na ujangili duniani kama moja ya shughuli zake kuu.
Moja ya hatua ambazo Prince Charles ameamua kuchukua ni kukabiliana na soko la bidhaa kuu za ujangili duniani, na hasa meno ya tembo na faru, na kufanya kampeni kubwa duniani dhidi ya biashara hiyo haramu.
Prince Charles ametoa pongezi hizo na msimamo wake wa kuunga mkono jitihada za Tanzania wakati alipokutana kwa mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. Viongozi hao wamekutana kwenye Jumba la Tintagel mjini Colombo, Sri Lanka, ambako amefikia wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola (CHOGM) ambao Prince Charles ameufungua rasmi asubuhi ya leo, Ijumaa, Novemba 15, 2013, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mahinda Rajapaksa.
Rais Kikwete naye yuko Sri Lanka kuhudhuria Mkutano huo. Wakati wa mazungumzo hayo, Rais Kikwete ametumia muda mrefu kumwelezea Prince Charles kuhusu hatua ambazo zimekuwa zinachukuliwa na Serikali yake kupambana na ujagili dhidi ya tembo na faru ikiwamo Operesheni Maalum – Operesheni Tokomeza -ambayo ilifanyika hivi karibuni kuwasaka na kukabiliana na wafanya biashara haramu ya meno ya tembo.
Rais Kikwete amemwambia Prince Charles kuwa pamoja na kuchunguza malalamiko yaliyotolewa na makundi mbali mbali ya watu kuhusu operesheni hiyo ya kwanza, bado operesheni hiyo itaendelea kwa sababu ni muhimu kulinda wanyamapori dhidi ya majangili. “Imefika mahali ambako tunahitaji kuchukua hatua kali.
Wakati wa Uhuru wetu kulikuwepo na tembo kiasi cha 350,000 lakini ilipofika mwaka 1989 idadi hiyo ilikuwa imepungua na kubakia 55,000. Hata hivyo, baada ya operesheni maalum na kubwa, idadi hiyo ilikuwa imeongezeka hadi kufikia 110,000 kabla ya kuanza wimbi jipya la ujangili mwaka 2010. Operesheni lazima iendelee,” Rais Kikwete amemwambia Prince Charles.
“Tusaidie kufunga na kuvuruga hili soko la bidhaa za wanyampori. Operesheni ya sasa imethibitisha kuwa mtandao wa uwindaji haramu na biashara haramu ya meno ya tembo na faru ni mkubwa na watu wengi wanahusika, lakini kinachovuruga zaidi ni kwamba lipo soko la uhakika la meno ya tembo.”
Prince Charles amemweleza Rais Kikwete kuhusu hatua ambazo anakusudia kuzichukua kukabiliana na hali hiyo, ikiwa ni pamoja na kuandaa mkutano mkubwa wa wakuu wa nchi na Serikali Februari 13, mwakani na kufanya mkutano mwingine mkubwa na vyombo vya habari kutoka pote duniani mwakani.
“Nakusudia pia kutumia wasanii nyota mbali mbali duniani kuendesha kampeni ya kuielimisha dunia kuhusu athari za biashara hiyo haramu kwa sababu asilimia kubwa ya mapato ya ujangili inasaidia kugharimia vikundi vya kigaidi duniani.”
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwana wa Malkia Elizabeth II wa Uingereza, Prince Charles, jijini Colombo, Sri Lanka, leo Novemba 15, 2013 pembeni ya mkutano wa Wakuu wa nchi za Junuiya ya Madola (CHOGM 2013) ambako Prince Charles, maarufu zaidi kama His Royal Highness the Prince of Wales, anamwakilisha mama yake mwenye umri wa miaka 87 ambaye hakuhudhuria kwa mara ya kwanza katika miaka 40 ya historia ya mkutano huo unaofanyika kila baada ya miaka miwili katika nchi itayoteuliwa mwishoni mwa mkutano. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe Peter Kallaghe.
Malkia Elizabeth wa II alihudhuria CHOGM kwa mara ya kwanza mwaka 1973 jijini Ottawa, akiwa kakosa kikao cha mwaka 1971, na tokea hapo hajakosekana tena hadi safari hii. Alikuwepo pia katika mkutano wa mwisho uliofanyika mwaka 2011 jijini Perth, Australia. Na hii ni mara ya kwanza kwa Prince Charles kumwakilisha mama yake ambaye imesemekana hakwenda Sri Lanka kutokana na ushauri wa kutosafiri umbali mrefu. Ila katika CHOGM 2007 iliyofanyika Kampala, Uganda, yeye na mama yake walihudhuria pamoja.
Sherehe
hizo zilizofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Nelum Pokuna Mahinda Rajapaksa
mjini Colombo, Sri Lanka, ziliendelea kwa karibu saa mbili kuanzia saa nne
kamili asubuhi.
Miongoni
mwa viongozi ambao walizungumza kwenye sherehe hiyo ya ufunguzi ni Rais wa
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kisoshalisti ya Sri Lanka, Mheshimiwa Mahinda
Rajapaksa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Mheshimiwa Kamalesh Sharma.
Mrithi
wa Kiti cha Ufalme wa Uingereza Prince Charles ndiye amefungua rasmi Mkutano
huo kwa niaba ya Mama yake, Malkia Elizabeth ambaye ni Mkuu wa Jumuiya ya
Madola. Malkia Elizabeth hakuweza kuhudhuria Mkutano huo.
Mara
baada ya ufunguzi huo uliopambwa na ngoma za kuvutia sana ukiwamo muziki wa
vijana na maonyesho ya watoto wa shule ambao walizunguka Ukumbi wa Mikutano,
wakuu hao walihamia kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kumbukumbu wa Bandaranaike kwa
ajili ya kuanza vikao rasmi.
Wakati
wa chakula cha mchana, viongozi hao walihudhuria hafla rasmi iliyoandaliwa na
Mheshimiwa Sharma na baadaye jioni wamehudhuria Chakula cha Usiku
kilichoandaliwa na Prince Charles na mkewe, The Duchess of Cornall kwenye
Hoteli ya Cinnamon Lakeside.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu, DAR ES SALAAM.
15 Novemba, 2013
Hongera JK kwa jitihada zako.leo nilikuwa nasoma legislation nchini uingereza nikakuta jinsi wanavyoshauri mabadiriko ya sheria hasa kunapokuwa na mabadiriko kadhaa duniani mf matumizi ya technologia,utandawazi na kadharika.nikafikiria nchi yangu inavyokuwa na utayari kisheria kuendana na mabadiriko kadhaa nikagundua kuwa kuna tatizo juu ya kubadili au kuanzisha sHeria mpya dhidi ya mabadiliko.mf utandawazi umeleta wimbi la wageni ambao wanakuwa macho na opportunities zilizojaa nchini ila vyombo vyetu vya kutunga na kusimamia sheria bado viko ndani ya usingizi wa ujamaa.hawa wachina wako dunia nzima na nchi kama uingereza zinao wengi tu na wahalifu wa kimataifa wamejaa ila kwa kuwa nchi iko macho kubadili na kusimamia sheria zake hawathubutu kufanya majanga kama wanayotufanyia.bunge letu mfano mpaka kutunga au kubadili sheria lazima kuwe na janga la kutikisa nchi.uwezo wa kukamata majangiri,kusaka wahamiaji haramu nk havihitaji mpaka JK aingilie kati wakati tunawalipa kodi zetu wajue ni kazi yao kila wizara.uwezo upo ila kila mmoja hatimizi wajibu.kwa utandawazi tutaona mengi.Rwanda iko mbali kiutandawazi ila inajisimamia kikamilifu na ukienda pale kigali utaona jinsi security ilivyo makini.ni wakati muafaka kila mmoja kutimiza wajibu kwa nafasi yake si mpaka Raisi aseme.Wabunge msifanye kazi kwa kutetea njaa kisiasa tu,polisi acheni kabisa Rushwa,Serikali wekeni mkakati unaoeleweka wa kupambana na Rushwa.kajifunzeni kwa majirani Rwanda.HASA KIKUBWA RAISI ASIMAMIE RUSHWA KWA SABABU SI TAKUKURU WALA POLISI WALA USALAMA WA TAIFA WANA UWEZO WA KUSIMAMIA RUSHWA BALI RAISI WETU JK UNAWEZA na umeonyesha mambo mengi makubwa kwa kipindi chako cha mwisho-Mungu akuzidishie
ReplyDeleteMdau UK
Kikwete, Kikwete, Kikwete !!!
ReplyDeleteKikwete oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee !
Wasiotaka wapasuke,na wajinyonge.
Kikwete juuuuuuuu !!!
Tanzania juuuuuuu !!!
Hongera !
ReplyDeleteImara !
Waaa !
Si mchezo Mhe.Raisi JK yupo high table bega kwa bega na Prince Charles Mwana wa Malkia wa Uingereza!, ni Daraja kubwa kwa kuwa hata ktk Maulid kuna High table yake ambapo 'Masheikh' wanao amanika hukaa mbele na pamoja!
Ninaomba Mhe. Raisi Jakaya Kikwete atendewe haki hii moja nayostahili, NI KUHAKIKISHA NDEGE 'PRESEDENTIAL JET' INAKUWA SAWIA MUDA WOTE KWA KUWA INATIA FEDHEHA SAAANA KIONGOZI WETU JK MWEYE HESHIMA KUBWA DUNIANI KWA SASA KUSAFIRI KWA NDEGE ZA KAIWADA ZA ABIRIA ZA KIBIASHARA!!!
Wewe unayesema kuwa Raisi yupo bega kwa bega high table na UK, hii ni kutokana na kwamba nchi zimepangwa kwa alphabetical order. UK, United Republic of Tanzania etc.
ReplyDeleteHata kwenye UN kiti cha Tanzania kipo between UK na USA.