Mhe. Naibu Waziri wa Maji, Dk. Binilith Mahenge ameendelea na ziara yake mkoani Dodoma katika kangalia utekelezaji wa miradi ya maji ya vijiji 10 katika Halmashauri hiyo kupitia mpango wake wa Big Results Now. Dk. Mahenge ametembelea miradi mbali mbali ikiwemo Ng’humbi, Kibaigwa, Ntomoko na Mkoka na kujionea maendeleo ya miradi hiyo hadi kufikia sasa. Dk. Mahenge ametembelea wilaya za Mpwapwa, Kongwa na Kondoa na anategemea kumaliza ziara yake leo Jumamosi.
. Mhe. NWMA, Dk. Binilith Mahenge akiwa katika chanzo cha maji,

   Ng’humbi.
Mhe. NWMA, Dk. Binilith Mahenge akiwa katika harakati za kukagua

    tanki la mradi wa maji wa Mkoka.
Mhe. NWMA, Dk. Binilith Mahenge akisikiliza maelezo akiwa juu ya tanki la kuhifadhi maji, mradi wa maji Ng’humbi.
Dk. Binilith Mahenge akiwa kwenye mradi wa maji Kibaigwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Heko Dr. Bilinith Mahenge!

    Ama kweli mzigo mkubwa abebeshwe Mnyamwezi!

    Ndio uzuri wa kumpa kazi mtu kulingana na Fani yake.

    Dakitari anawajibika yeye mwenyewe kuhakikisha kama kazi imetendeka vyema!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...