Na Anna Nkinda- Maelezo
Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) kwa kushirikiana na Utepe wa Pink Utepe Mwekundu (PRRR) wanatarajia kuanza kufanya kazi kwa pamoja ya kuhakikisha kuwa ugonjwa wa saratani ya shingo ya uzazi na matiti unapungua au kuisha kabisa hapa nchini .
Hayo yamebainishwa leo wakati wa mazungumzo baina ya Wafanyakazi wa Taasisi ya WAMA wakiongozwa na Mwenyekiti wao Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Ujumbe kutoka Utepe wa Pinki Utepe Mwekundu yaliyofanyika katika ofisi za WAMA zilizopo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji kutoka Utepe wa Pinki Utepe Mwekundu Dk. Doyin Oluwole alisema jambo la muhimu ni kuangalia jinsi gani wanaweza kufanya kazi kwa pamoja na kuweza kuudhibiti ugonjwa huo ambao unawatesa wanawake wengi hapa nchini.


.bmp)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...