WAKATI maandalizi ya Tamasha la Krismas yakipamba moto, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mizengo Kayanza Peter Pinda amesema wazo la kuanzishwa kwa Tamasha la Krismas ni zuri lenye lengo la kuwakutanisha Watanzania mahali pamoja kuabudu na kuliombea Taifa lao dhidi ya mabalaa yanayoitesa dunia likiwemo suala la ugaidi, utekwaji wa viongozi na kuteswa kwa Watanzania.

Waziri Mkuu Pinda ambaye ni maarufu kama mtoto wa Mkulima anasema kwamba Tamasha hilo ni zuri na litakata kiu ya mashabiki wa Muziki wa Injili nchini tanzania kwa sababu linawakutanisha kwenye uwanja mmoja waumini wa madhehebu mbalimbali.

Waziri Mkuu anasema tamasha hilo ambalo wazo la Muandaaji maarufu wa Matamasha ya Injili nchini, Alex Msama linapewa baraka zote kwa niaba ya serikali kwa kuwa lengo lake kuu ni kuwafanya Watanzania kuwa na hofu ya Mungu katika maisha yao yote wanayoishi hapa duniani.

SOMA ZAIDI HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...