Habari iliyoifikia Globu ya Jamii hivi punde toka jijini Arusha,inaeleza kuwa Ndege ya abiria aina ya Boeing 767 ya shirika la ndege la Ethiopia (Ethiopian Airlines) mchana huu imeshindwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kutoka na hitilafu iliyokuwepo Uwanjani hapo na kulazimika kutua kwa dharula kwenye Uwanja wa Mdogo wa Arusha.
Wataalam wa Ndege wapo eneo la tukio hivi sasa kutafakari namna watakavyoweza kuwashusha abiria hao na kutafuta namna ya kuweka sawa mambo ili Ndege hiyo iweze kuruka.
Ndege hiyo ilikuwa na abiria zaidi ya 200 na wafanyakazi 9. kabla ya kupaa tena ilibidi abiria wote wateremke, na kupunguzwa mafuta ili kupunguza uzito wa ndege hiyo. Abiria waliamuriwa kwenda kupandia ndege hiyo kwenye Uwanja wa Ndege wa KIA.
Globu ya Jamii inaendelea kufatilia kwa ukaribu tukio hilo,na tutaendelea kufahamishana kadri taarifa zitakavyokuwa zikitufikia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. Mjomba sio boeing 787 ni boeing 767-383ER

    ReplyDelete
  2. Kuna watu lazima wawajibishwe kwenye hili. Kwann wasi clear runaway na badala yake kuidirect ndege kubwa kwenye uwanja mdogo. Itarukaje ss?

    ReplyDelete
  3. ni aibu sana kwa nchi yetu. Ni hitilafu gani hizo zilitokea uwanjani? Kuwepo miundombinu mibiovu Tanzania ni Matokeo ya ufisadi!

    ReplyDelete
  4. Ebu tuacha siasa,Rubaoteni alitakuwa kuwa na mafuta ya ziada yatakayo mwezesha yeye na ndege yake kutua kiwanja kinachoweza kuhudumia hiyo aina ya ndege yake, Endapo kukatokea dharula yoyote, Iyo ndege iliyokuwa kwenye Runway aikokotwi kama magari au baiskeli, kuna taratibu za kufanyika hapo. Pongezi kwa Rubani kwa kuweza kunusuru uhai wa abiria wote hayo mengine ni makosa ya kibinadamu...

    ReplyDelete
  5. Hii ndege ni kubwa sana....kwa kutua kwa dharura Arusha bila kupoteza maisha ya Abiria ni jambo nzuri...ila sasa kiuchumi inatuharibia

    ReplyDelete
  6. umasiki wa mawazo ni moja ya tatizo kubwa kuliko yote,kazi za kupeana ndiyo madhara yake,

    ReplyDelete
  7. msilalamike airlines wakikata safari za kuja bongo. kwa mwendo huu kama mimi ningekuwa investor ningekata safari za ndege zangu. hii inadamage reputation ya brand yako kwa customers.

    ReplyDelete
  8. Nimeona gari za zimamoto kwanza nikacheka hahahahaha wamekimbilia utadhani wana maji ya kutosha....yaani pale wameshukuru kweli...Bongo bwana tunasonga kibahati bahati tu.

    ReplyDelete
  9. Mikausho MikaliDecember 19, 2013

    Nashauri kabla hujaandika mtafutage ushauri wa watu wanaojua aviation :
    1.Gari la kusukuma ndege halipo KIA wala Arusha airport.Lazima litoke Nairobi au Dar
    2.Kwa case hiyo ndege lazima itolewe na Boeing test pilots tu na si vinginevyo.Pia itafunguliwa viti vyote ,watoe mizigo yote
    3.Ukishadeclare fuel emergency lazima uchanguzi ufanyike.ikibainika kwamba ulikuwa na mafuta machache kama walivyofanya hawa jamaa , marubani wananyang'anywa leseni na hata hilo shirika kufungiwa kutua nchini

    kwa hiyo nakataa hayo maelezo kwamba abiria walielekezwa kwenda kupandia ndege hiyo KIA.ungesema walielekezwa kwenda kupanda ndege nyingine KIA

    ReplyDelete
  10. sio kazi tu hata vyeti vya kupeana Hivi hawa waongozaji ndege pale airport wanasoma wapi. Lakini kwani kama kuna hitilafu airport si ndege inazunguka baandae inaruhusiwa kutua. Sasa mnaanza kutoa mbaya bila ya kujua taratibu za uongozaji ndege.

    ReplyDelete
  11. Wabongo ni wababaishaji tu. Lazima makosa yatakuwa yametokana na uzembe wa wabongo. Haya sasa image ya nchi inapotea, watalii wanaweza wasije tena maana usafiri utakuwa wa shida kama ndege zitakataa kutua KIA. SHAME ON YOU wababaishaji wa Tz.

    ReplyDelete
  12. Pongezi kwa rubano,ila Nachojiuliza ni jinsi gani Ndege hiyo itakavyoondoka uwanjani hapo,cause kwa taarifa ni kwamba uwanja una 1.1mile while ili ndege hiyo iweze kupaa inahitaji Njia ya urefu Wa 2.5 miles.

    ReplyDelete
  13. Ethiopian Airlines booking Grab cheap Ethiopian airlines flight tickets, pay less - save more. No hidden charges.

    ReplyDelete
  14. Ethiopian Airlines booking Grab cheap Ethiopian airlines flight tickets, pay less - save more. No hidden charges.

    ReplyDelete
  15. Ethiopian Airlines booking Grab cheap Ethiopian airlines flight tickets, pay less - save more. No hidden charges.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...