Mwanamke wa Kitanzania mwenye umri wa miaka 28 amekutwa na kilo 1.1 za madawa ya kulevya aina ya heroin alizokuwa amezihifadhi tumboni mwake,baada ya kukamatwa huko Macao, nchini China. Dawa hizo zenye jumla ya vidonge 66 vinakadiriwa kuwa na thamani ya dola za Kimarekani 137,720.

Mwanamke huyo alikuwa akisafiri kutoka Thailand akielekea Macao Jumanne iliyopita. Aliwaambia polisi kuwa alikuwa anaelekea Guangzhou ambao ni mji wa jimbo la Guangdong huko Chima.
Pichani ni mwanamke huyo wa Kitanzania (akiwa amefunikwa uso) aliyekamatwa na kilo 1.1 za heroin huko Macau. Hapo amepigwa picha na vidonge vyake wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari mjini Macau, Disemba 19, 2013.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 21 mpaka sasa



  1. wewe muandishi macau na china vitu viwili tofauti kabisaaa macau is a part of hongkong and not china
    rekebisha sema MACAU,HONG KONG

    alafu huyo mwanamke ni mjinga maana siku hizi ukiwa umetoka BKK kuingia HKG lazima upigwa xray pole yake

    ReplyDelete
    Replies
    1. Macau na HK ni nchi moja ya China mwandishi yupo sawa, sema hizo sehemu mbili ni majimbo huru chini ya China. Yanajitegemea kwenye ulinzi na mambo ya nje. Vile vile yote yalikuwa chini ya ukoloni wa ureno(macau) na HK(uingereza). Na ndo mana China wana sheria ya kunyonga Kwa kusafirisha unga wakati sehemu huru wana sheria zao tofauti.

      Delete
  2. Ajari kazini!Jasho litamtoka china!

    ReplyDelete
  3. Ndio mambo safari hii amebambwa. Kama angevuka basi ni millionea akirudi Bongo. Je Macau wana sheria ya kunyonga?

    ReplyDelete
  4. Mie napenda kweli wakishikwa. Sema hii nchi hawanyongi, wangewanyonga tu yaishe, hajaanza leo wala jana, kujiringisha na mapicha ya cl na brand bags, wenyewe wanaita no fake zone, kumbe kazi ni kuuwa wenzae. My uncle was a drugg addict alikuwa anatuibia mpaka vijiko ili apate hela ya unga, mkifua inabidi mlinde kwa kupokezana maana keshaiba sana nguo ili apate hela ya unga.
    Huyu dada ni full maonyesho na alishawahi kuulizwa kama anauza unga akijibu kuwa ye ni mzuri hawezi uza unga, leo kiko wapi full kandambili badala ya CL.
    Wanatuchafua sana sasa hivi kila tunakopita tunanuka.

    ReplyDelete
  5. Mungu wangu!

    Ohhh haya maisha ya juu bila Mipango ya maana kwa ndugu zetu akina dada wa Kitanzania yatafanya wasichana wooote warembo kuishia Magerezani nje ya nchi!!!

    ReplyDelete
  6. Hapo katika hizo US Dola 137,720 utakuta yeye Punda hata US Dola 10,000 ni tabu kulipwa kama Mshahara wake na huyo Bosi wake aliyemtuma !

    ReplyDelete
  7. she has sealed her fate, death by firing squad, how sad!

    ReplyDelete
  8. Ya nini tabu?

    Ya nini kuchezea Kifungo Kirefu Gerezani ama kuhukumiwa Kifo?

    Isiwe tabu, Tanzania ina Fursa nyingi mno za kuyapata Mapesa ni kufunguka kiakili utaziona !

    1.Kilimo cha Kisasa,
    2.Biashara ya Madini,
    3.Ujasiriamali wa kawaida,
    4.Huduma za Kibiashara ikiwemo Lishe na mengineyo,
    5.Mauwa na Urembo,
    6.Mazao ya Maliasili,
    7.Uwakala wa Huduma
    -Vocha za Simu za Jumla
    -Maji na Bidhaa za Vyakula vya Viwandani (Bakhresa, Metl, n.k)

    FURSA HIZO 7 HAPO JUU KWA UCHACHE WAGENI HARAMU WANAINGIA TANZANIA NA KUZICHANGAMKIA HADI Mhe.RAISI KIKWETE ANAWATIMUA NA OPERESHENI KIMBUNGA!

    JAMANI KAMA WAO WAMEWEZA WANA NINI, NA SISI TUKISHINDWA TUNA NINI?

    WAKATI NCHI NI YETU NA FURSA NI ZETU HADI TUKAUZE MADAWA UGENINI NA KUTUGHARIMU KIFO AMA KIFUNGO KIREFU?

    ReplyDelete
  9. Ohhh masikini weee ndugu yetu!

    Amesema ngoja nijaribu kidogo haka kamzigo ka Kilo moja na GrAMU 100 labda nitafanikiwa MATOKEO YAKE SASA ANACHUNGULIA KABURI!!!

    ReplyDelete
  10. Maisha ya juu yanaponza!

    Ili kubakia kukaa juu siku zote wanalazimika kuuza Madawa ya kulevya.

    Heri mimi nimeridhika na Dona langu kwa dagaa chungu la Kigoma kwa akina Diamond Plutnumz!!!

    ReplyDelete
  11. Jamani katika ni hivi,

    1.Michezoni kwenye Usajili wa Ligi kuna Usajili Mkuu na pia Dirisha Dogo la Usajili!,

    2.Maisha pia kama ilivyokuwa Michezo yana Plan-A na pia Plan-B, kama Plan-A inakuwa ngumu ni vema kuchukua Plan-B!

    Tuachane na maisha ya kutaka mafanikio makubwa na kwa haraka, twende mwendo wa Pole Mwenyezi ni Tajiri sana atatupa tu!

    Tusije kwisha kwa kunyongwa Ugenini maana nchi zingine sio kama kwetu pana Mipango mipango huko hata Hongo hakuna ukishikwa ni Kisu kooni tu!

    Tuangalie Mipango mbadala ya kufikia malengo ya kimaisha na tuachane na kasi ya kuifukuza Sarafu!!!

    ReplyDelete
  12. WATU HAWAKOMI!! KUNA WA WATU KIBAO DAR NA WAKE ZAO WANAJENGA MAJUMBA KWA BIASHARA HII WAKIDHANI NDIO MAISHA MAZURI. SINA HURUMA KABISA NA WATU HAWA.

    ReplyDelete
  13. wapenda njia za mkato. Na shule labda walikuwa wanataka maksi bila kusoma.

    unajuwa hiyo ni njia ya mkato kwenda kaburini, jamaa sheria yao ni kifo.

    ReplyDelete
  14. Masikini weee Dadetu alijipigia mahesabu yake hiyo tarehe 19 Disemba, 2013 anamaliza Mazagazaga ya biashara yake MKWANJA KIBAO MKONONI US$ 137,170 KUZITIA KIBINDONI kutoka kwa hao macho madogo (China) halafu ile tarehe 24 Disemba , 2013 mchana wa mapema anatua nyumbani Dar-Bongo kuja kuanza Mkesha wa Krismasi!

    Haikuwa hivyo, dadetu anajikuta KRISMASI mwanawane yupo CHINA tena LUPANGO !

    ReplyDelete
  15. Why are so growing to give up our freedom for money, very disappointing!!!!

    ReplyDelete
  16. Majanga!, jamani majanga!

    Dada yetu anapigania mpango wake tena tarehe za Krismasi ili achane zake bata baada ya kupata Fwedha, ohhh anajikuta pwaaa chini ya Ulinzi China anavikwa Ninja Jeusi kichwani na Pingu mikononi !,,,Kizibiti ubaoni na Wanalibeneke hewani mapicha kwacha kwacha bila chenga live.

    Ama kweli mwaka wa balaa 2013 namna hii unaisha kwa msala?

    ReplyDelete
  17. Tujikhalifu nafsi zetu kwa kuanza maisha mapya kwa kazi za Kuchoma maandazi na vitumbua na kunaanga mihogo!

    Masuala ya Biashara hizi za Madawa tutakwisha, Mchina ananyonga sana hata Umoja wa Mataifa na Amnesty International wameilalamikia sana, lakini wapi msimamo wao upo pale pale KISU, BASTOLA , KITANZI!

    Maana Viwanja vya ndege dunaini vimekuwa vigumu hakupitiki kabisaa tutanyongewa ndugu zetu sana !

    ReplyDelete
  18. Mchangiaji wa kwanza hapo juu, Unakosoa kumbe unakosea. Mwaandishi alichokiandika ni sahihi na kwa taarifa yako Hong Kong na Macau zopte ni mamlaka ya China ni sehemu ya Jamhuri ya watu wa China. Macau ilitawaliwa na wareno na Hong Kong na waingereza. Zote mbili zimerudishwa katika mamlaka ya China ambayo inaendelea pia kuidai Taiwan.

    ReplyDelete
  19. demu mwenyewe mbona kama mzungu tena

    ReplyDelete
  20. Understandably mdau wa 20 amekasirika sana but hamna haja ya matusi. I m surprised ndugu Michuzi has published the comments. Anyway, whatever the punishment this woman is going to get is not enough. Madawa haya yanaharibu watoto wa watu. It destroys families. It kills people be it Tanzanians or otherwise. Can u imagine how this womans ndugu feels? Inawezekana ana katoto pia. Masikini ya Mungu. Jamani tamaa ni mbaya. Utajiri wa haraka haraka hauna baraka. We have a beautiful fertile country. Use it to make a healthy living please... message to those who have same plans as this unfortunate woman.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...