Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya awali ya ukocha waliokabidhiwa vyeti vya kozi hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na vyeti vyao. (picha zote na Denis Mlowe).
 Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya awali ya ukocha waliokabidhiwa vyeti vya kozi hiyo kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa shule ya kimataifa ya Southern Highland Kitova Mungai.
 Mwenyekiti wa Chama cha Soka Wilaya ya Mufindi Gervas Choga akimkabidhi cheti ya kozi ya awali ya ukocha Lupyana Massawe, kulia ni mkurugenzi wa Hazina Foundation William Mungai makabidhiano yaliyofanyika katika ukumbi wa John's Corner mjini Mafinga. 

==========  =========  ===========

WAKABIDHIWA VYETI VYA UKOCHA WA AWALI

Na Denis Mlowe, Mufindi

ASASI isiyo ya Kiserikali ya Hazina Foundation iliyoko Mafinga imekabidhi vyeti 26 kwa wahitimu wa kozi ya awali ya ukocha kwa walimu wa Shule za Msingi na Sekondari wa Wilaya ya Mufindi.

Akikabidhi vyeti hivyo Mwenyekiti wa Chama cha Soka Wilaya ya Mufindi Gervas Choga aliwataka wahitimu hao kwenda kuvumbua vipaji vilivyojificha mashuleni na kuwaendeleza soka katika wilaya ya Mufindi.

Alisema mafunzo waliyopata ni muhimu sana kwa maendeleo ya soka la wilaya ya hiyo na taifa kwa ujumla na serikali inatakiwa kuwekeza  katika michezo na kuondokana na siasa iliyotawala sasa kwa watu wengi kujiingiza katika mpira kwa lengo la kupata umaarufu na mwisho kujiunga katika siasa.

Choga alisema vipaji vya soka vinaanzia shule za msingi hivyo ni jukumu la kila mmoja wenu kuweza kuandaa michezo ya kila mara katika shule mnazofundisha na maeneo yanayowazunguka.

“Nitahakikisha kila mmoja wenu anayafanyia kazi mafunzo haya na hakuna hata mmoja nisiyemjua hivyi katibu nakuagiza wafatilie wahitimu hawa na kuona wanafanya jambi kuhusu soka la wilaya yetu linakuwa, naomba vijana mtusaidie katika kuendeleza soka kwa kupitia mafunzo mliyopata” alisema Choga

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Hazina Foundation,William Mungai aliwataka wahitimu kuyatendea haki mafunzo hayo kwa kuwafundisha watoto mpira wa kisasa kuweza kufikia malengo ya kukuza soka la Mufindi na Taifa kwa ujumla.

Wiliam Mungai alisema mafunzo ya ukocha yatakuwa endelevu kwa walimu na wadau mbalimbali watakohitaji kujifunza ukocha ngazi ya awali na asasi ya Hazina itagharamia mafunzo hayo kwa vijana wa wilaya hiyo.

Alisema mafunzo hayo yanatakiwa kuanzia ngazi ya chini na bila kubagua jinsia kwa  kufundisha vijana wenye uwezo n kuthamini mpira wa miguu kunakuwa na faida kubwa na manufaa kwa vizazi vijavyo

Wiliam Mungai iliitaka serikali kuwekeza katika vyuo vyingi vya ufundishaji michezo kwa faida ya miaka ijayo katika kukuza michezo na kuongeza pato  la Taifa.

“Naomba sana  vijana wangu mwende mkafundishe soka la kisasa kwa vijana wetu nategemea sana kila mwaka kuongezeka kwa vipaji katika wilaya yetu na msiishie hapa na kozi hii ya awali mjiendeleze katika fani  yenu na kama mnavyojua soka la Tanzania kwa sasa lipo nyuma sana so tuanzie huku chini kwa kuibua vipaji vya kutosha” alisema Willam Mungai.

Mafunzo hayo yalioendeshwa na Kocha Bonifas Mkwasa mwezi Juni 25 hadi Julai 6  mwaka huu kwa udhamini mkubwa wa asasi ya hazina Foundation inayomilikiwa na Wiliam Mungai na makao makuu yako mjini Mafinga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...