Mgeni rasmi ambaye ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga akiwasalimu Wanabonanza wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Dar es Saalam(hawapo pichani) kwa Kauli mbiu ya "Familia Kwanza" kabla ya kuzindua rasmi "Family Bonanza" lililoandaliwa na Maofisa, Askari wa Jeshi la Magereza wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Dar es Salaam pamoja na familia zao. Bonanza hilo limejumuisha Michezo mbalimbali ikiwemo Mpira wa Wavu, Mpira wa Pete, Mpira wa Miguu, Kukimbia na Gunia na Kuvuta Kamba.
Bendi ya Jeshi la Magereza ikiongoza Maandamano Maalum yaliyoandaliwa na Wanabonanza wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Dar es Salaam wakiingia rasmi katika Viwanja vya Michezo vya Chuo Ukonga kabla ya uzinduzi rasmi wa Bonanza hilo ambalo limezinduliwa leo Januari 04, 2014 na Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga
Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga akikagua Kikosi cha Timu cha Maafisa na Askari wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Dar es Salaam kabla ya kuchuana vikali na Timu ya Wanafunzi wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga wanaosomea Stashahada ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam leo Januari 04, 2014 katika Viwanja vya Michezo vya Chuo hicho.
WakinaMama wa Kambi ya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga wakichuana vikali katika Mchezo wa kuvuta kamba iliyowahusisha na Maafisa Wanawake wa Jeshi la Magereza wanaofanya kazi Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Dar es Salaam leo katika Bonanza hilo.
WakinaMama wa Kambi ya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga wakichuana vikali katika Mchezo wa kukimbia na Gunia wakati wa "Family Day Bonanza" lililohusisha Maofisa, Askari pamoja na familia zao. Bonanza hilo limefanyika leo Januari 04, 2014 katika Viwanja vya Michezo vya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Dar es Salaam(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
mwanzo mzuri. safi sana mhabarishaji wetu. safi sana michuzi blog
ReplyDelete