Viongozi wa dini wametembelea Bomba Jipya la Gesi asilia la Mtwara- Dar es Salaam, mtambo wa kusafisha umeme wa Mnazi Bay na maeneo mengine mbalimbali ya uendelezaji wa gesi asilia katika Mkoa wa Lindi na Mtwara. Viongozi hao wamefanya ziara hiyo ikiwa ni maandalizi kabla ya kufanyika Kongamano la Viongozi wa dini linalotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam tarehe 21 na 22 mwezi Januari, 2014.
Ujumbe wa Viongozi wa dini wakiangalia mojawapo ya visima vya nchi kavu vya kusafisha gesi katika eneo la Mnazi Bay, Mtwara.
Viongozi wa dini wakipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Masuala ya gesi na Msimamizi Mkuu wa Mitambo ya kusafisha gesi Mhandisi Sultan Pwaga katika eneo la Madimba kinapojengwa Kiwanda cha kutakasa Gesi.
Mafundi wa Kampuni ya China Petroleum Pipline (CPP) wakiendelea na kazi ya kuunganisha mambomba ya gesi katika kambi ya Madangwa.
Meneja Mradi wa Bomba la gesi kutoka Da r es Salaam hadi Mtwara Mhandisi Kapuulya Musomba akiwaeleza viongozi wa hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa Mradi huo. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Usalama wa Bomba la Gesi dhidi ya hujuma:

    Mambo mawili hapa chini ni muhimu sana,

    1.Njia nzima linamopita Bomba la Gesi yawekwe makubaliano na google Satelite map, ili waiingize ktk Ramani na camera kwa kila dakika inayokwenda.

    2.Iwekwe ktk Makubaliano na FLUID LEAKING TECHNOLOGY yaani Taasisi inayotoa Tekinolojia ya uvujai wa vitu vya gesi/ hewa na maji Mamlaka inaweka software zao ku detect tukio lilipotokea na kutuma mawimbi ya taarifa kwenye Kituo.

    Bila ya hatua hizi mbili hata kwa gharama kidogo nina wasiwasi na usalama wa bomba la gesi dhidi ya hujuma kwa kuwa maeneo mengine linapita misituni kabisa!!!

    ReplyDelete
  2. Mdau wa kwanza:

    Hilo ni muhimu kulingana na uzito wa suala lenyewe na jinsi changamoto zilivyo jitokeza hasa kwa wakazi wa eneo hilo la mikoa linakopita Bomba la Gesi kuhusiana na mpango huu.

    ReplyDelete
  3. Mdau wa kwanza,

    Ni kweli kabisa kwa kuwa hata ktk familia mtazaliwa wengi lakini hapawezekani kila mmoja akawa na akili timamu lazima moja wapo litakuwa NDONDO tu!

    Ndio hivyo hivyo hata kwenye nchi, hamuwezi wote kuwa na akili nzuri lazima utakuta panajitokeza Miteja na Mivibaka ya kuiba hadi mifuniko ya mitaro ya majitaka barabarani, kung'oa mataruma ya Reli na mawaya ya transfoma kuwenda kuuza Skrepa!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...