Kinana akisoma vijiji vitavyopata umeme wilayani Sikonge mwaka huu wa fedha.
 Katibu Mkuu  wa CCM, Kinana akihutubia katika mkutano huo leo Mei 15, 2014, ambapo akijibu Malalamiko ya Wananchi wa Kata ya Kitunda, alielezea kusikishwa kwake na kitendo cha vyama vya ushirika kudaiwa kuwadhulumu bila huruma wakulima wa tumbaku wa Kata hiyo, huku akionyesha kushangazwa kwake na hatua ya  waziri mwenye dhamana na kilimo, Chakula na Ushirika kutotembelea wakulima kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi. Mapema baadhi ya wananchi waliopata fursa ya kuuliza maswali au kutoa maoni kuhusu kero  walidaikuwa zaidi y  asilimia 64 ya wakulima hawajapewa malipo yao ya mauzo ya tumbaku ya mwaka jana na vyama vya ushirika katika Kata ya Kitunda, wilayani Sikonge, mkoani Tabora. Pia wakulima hao walisema kuwa wanadaiwa zaidi ya sh. bilioni 112 za mauzo hewa ya  pembembejeo.
 Mkulima wa tumbaku katika Kata ya Kitunda, wilayani Sikonge, akielezea mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana jinsi viongozi wa vyama vya ushirika walivyosaini mkataba hewa wa pembejeo zenye thamani ya s dola za kimarekani 150.
 Mwakilishi wa wakulima wa tumbaku katika Chama cha Ushirika  cha Tumbaku Mkoa wa Tabora ( WETCO), Lameck Mnyama, akielezea  jinsi viongozi wa ushirika huo wanavyowanyonya wakulima wa zao hilo, wakati wa mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kitunda uliohutubiwa na Katibu Mkuu wa CCM ambapo alidai hadi sasa wanaudai ushirika dola za kimarekani 76. Picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 16, 2014

    MKOA WA TABORA UMESAHAULIKA SANA SANA, UKIACHA IGUNGA NA NZEGA HAO WALIOKO HUKO NDANI KWELI HALI YA MAENDELEO SI NZURI AND NJIA MBADALA NI NYIE WATANI ZETU, MSISAHAU BARABARA!!! WAJENGE BARABARA HIYO HAIWEZEKANI MIAKA 51 YA UHURU HAMJAWAHI KUWA NA MAENDELEO. ITOKE TABORA MJINI MPAKA MPANDA WASILETE SIASA ZA MANENO MATUPU IWE KWA VITENDOOOO.....! TUMBAKU IMEANZA KULIMWA HUKO TOKA ENZI; BARABARA NI KITU MUHIMU SANA. DUH, HEBU WEWE FIKIRI TOKA PUGE KUPITIA NDALA MPAKA TABORA MJINI VUMBI.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...