Miss Universe Tanzania 2007 na mwanamitindo wa kimataifa Flaviana Matata leo amejumuika na wananchi wengine mkoani Mwanza katika Ibada maalum ya kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya kuwaombea marehemu waliopoteza maisha yao baada ya kuzama kwa meli ya Mv Bukoba miaka 18 iliyopitta.  
 Flaviana Matata, ambaye anafanyia shughuli zake   nchini Uingereza na Marekani ni mmoja wa watu  waliopoteza ndugu zao kwenye ajali hiyo. Yeye alimpoteza mama yake mzazi na Kaka yake. Mbali na kusindikizwa na ndugu jamaa na marafiki pia alisindikizwa na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani  Mhe. Mwanaidi Maajar pamoja na wasanii maarufu kadhaa akiwemo AY.
  Ajali ya kuzama kwa Mv Bukoba ilitokea katika ziwa Victoria mnamo tarehe 21/5/1996 na kupoteza maisha ya zaidi yawatu 1000.
Ukiondoa mrembo huyo Misa hiyo pia imehudhuriwa na viongozi wa dini, ndugu wa karibu wa Flaviana akiwemo baba yake Mzazi, Marafiki zake, wananchi mbalimbali na pia Viongozi wa serikali kupitia kampuni ya Marine Services Company Limited ambayo imekuwa ikifanya hivyo kila mwaka.
Ibada hiyo fupi imefanyika katika makaburi ya Igoma ambapo ndipo walipozikwa na tukio hilo kama kawaida litaambatana na shughuli ya kuweka mashada ya maua na kuwasha mishumaa. Flaviana na Balozi Mwanaidi Maajar walishiriki kuweka mashada katika mababuri Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ambwene Yesaya almaarufu kama AY alikuwepo kuungana na Flaviana Matata Baba Mzazi wa Mwanamitindo huyo nae alikuwepo kwenye misa ya kuwaombea

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 22, 2014

    Rafiki yetu mpendwa Lydia tunakukumbuka na kukuombea mapumziko mema pamoja na mwanao.

    Mollel

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 22, 2014

    POLE FLAVIANA MATATA NAJUA MAMAKO ALIKUFA KATIKA AJARI HII MBAYA.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 22, 2014

    Pole sana watanzania. Lakini tuwe taari kwani hatujui siku wala saa ya kijiliwa. Tuwe taari na tujitakase na kukaa sawasawa na MUNGU aliye hai.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...