Balozi wa maziwa makuu nchini Kenya katika wizara ya mambo ya nje, Mhe. Muburi Muita(aliyenyoosha mikono) akiongea na Katibu mkuu wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel wakati alipomtembelea ofisini kwake na ujumbe wa kutoka eneo la maziwa makuu(ICGLR) waliokuja kuangalia ushiriki wa vijana katika uchaguzi mkuu wa Tanzania na kuelezea kufurahishwa na ushiriki wa vijana wengi katika uchaguzi huu na kwamba uchaguzi ulikuwa wa Amani na mafanikio makubwa.Ujumbe huo unajumuisha nchi za Zambia,Burundi,Kenya,Congo,Uganda na Sudan.
Katibu mkuu wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel(wa pili kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya  pamoja na ujumbe wa maziwa makuu ambao upo nchini ukiangalia ushiriki wa vijana katika uchaguzi mkuu wa Tanzania.Wengine kwenye picha ni  Balozi wa maziwa makuu nchini Kenya katika wizara ya mambo ya nje, Mhe. Muburi Muita(wa kwanza Kushoto waliokaa) na Nancy Kaizilege wa Umoja wa mataifa Tanzania.(wa kwanza kulia waliokaa).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...