UD1
Mwenyekiti wa Jumuiya ya kukusanya Zaka na Sadaka Zanzibar (JUZASA) Shekh. Said Masoud (Gwiji) akitoa maelezo ya Jumuiya na kumkaribisha mgeni rasmi (kushoto) Katibu Mtendaji Kamisheni ya Wakfu na Mali ya amana Zanzibar Shekh. Abdalla Talib kufungua Mkutano wa Jumuiya hiyo uliofanyika katika ukumbi Sha-Ntimba Mombasa Zanzibar.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanziba
UD2
Baadhi ya wanachama wa Jumuiya na wageni walikwa wakisikiliza nasaha za Mwenyekiti wa Jumuiya ya kukusanya Zaka na Sadaka Zanzibar (JUZASA) Shekh. Said Masoud (Gwiji) hayupo pichani wakati wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya hiyo.
UD3
Mjumbe wa Bodi ya Jumuiya hiyo Dkt. Muh’d Hafidh akitoa neno la shukrani mara baada ya kumaliza kwa Mkutano. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.  
………………………………………….
Na Maelezo Zanzibar.

Taasisi za kiislamu nchini zimeshauriwa kushawishi kuwepo kwa mfumo wa pamoja wa ukusanyaji wa Zaka na Sadaka ili ziweze kuleta tija katika kundi kubwa la jamii ya Kislam.

Katibu mtendaji wa kamisheni ya mufti namali ya amana Zanzibar sheikh abdalla talib amesema Lengo la mfumo huo uliwekwa kwa mujibu wa sheria za kiislamu ni kusadia na kupunguza umasikini katika jamii lakini kwa sasa wengi wanaotaoa sadka hizo hazifikii lengo hilo kwa vile kumekosekana mfumo bora  unaowafikia watu wengi na kuleta mabadiliko makubwa.

Akifungua mkutano wa jumuiya ya zaka na sadaka Zanzibar ZASA ametolea mfano wan chi ya denmar amabyo ina waislamu kwa asilimi 3 tu imekuw ana utaratibu mzuri wa ukusanyaji wa sadka na zaka  hali iliyofanikisha kupatikana  misaada mingi iliyosaidia  katika nchi hiyo na hata nchi nyengine.

Amefahamisha kuwa  kwa kuwa  Zanzibar asilimia kubwa ya wanananchi wake ni waislamu ina nafasi ya kufikia malengo hayo kama pia itatoa elimu kwa wananchi hasa wenye uwezo  ili kufahamu  umuhimu wa Ibada hiyo pamoja na njia bora za kutoa zaka na sadaka katika jamii.
Nae mwenyekii wa jumuiy hiyo sheikh said masoud  amesema kwa sasa umekuwa na mwamko mdogo hasa kwa wafanyabiashara kutoa zaka na sadaka  kulingana na taratibu zinazotakiwa  kidini.

Nae katibu wa jumuiya hiyo ya jusaza omar abubakar Mohamed amesema jumuiya hiyo  imeshatoa zaka kwa watu 46 zikiwemo za fedha taslim, charahani, friza na wengine kujengewa nyumba.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. NAOMBA KUWA MJUMBE WA JUMUIYA YA KUTOA ZAKKA NA SADAKA ILI TUWEZE KUSHIRIKIANA .
    AHSANTE

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...