Na Bakari Issa Madjeshi

Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) limekataa rufaa ya  Rais wa Shirikisho hilo ambaye anatoka madarakani, Sepp Blatter na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Ulaya (UEFA) aliyesimamishwa kazi, Michael Platini.
Kamati ya Rufaa ya FIFA imekataa rufaa ya Marais hao lakini imewapunguzia adhabu ya kujihusisha na masuala ya soka kutoka miaka nane hadi miaka sita.

Wote walipatikana na hatia ya matumizi mabaya ya fedha kiasi cha Paundi Milioni 1.3 sawa na Dola Milioni 2 ambazo Blatter alimlipa Platini kwa kile walichokiita kazi maalum.

Blatter na Platini walikataa kufanya hivyo na kusema  kuwa wanakwenda katika Mahakama ya Rufaa  (CAS) kukata rufaa.
Pia wamesema  makubaliano ya malipo ya mwaka 1998 yalikuwa  yakiungwana kwa kazi iliyofanywa na  Mfaransa huyo wakati alipokuwa mshauri wa ufundi wa Blatter.

Hata hivyo,Blatter katika maelezo yake alieleza kuwa “sijakubaliana na Kamati ya Rufaa ya FIFA”.

Naye,Platini alisema kuwa “ni udharirishaji na aibu kwa maamuzi hayo ya kisiasa”.

Uchaguzi wa kumtafuta mbadala wa Blatter utafanyika siku ya Ijumaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...