Na  Bashir  Yakub

1.LESENI  HUTOLEWA  KWA  NAMNA  MBILI.
Unapohitaji  leseni  ya  kutafuta madini  unapaswa  kujua  kuwa  leseni  hizi  hutafutwa  kwa  namna  mbili  tofauti. Kwanza  kwa  maombi  maalum  na  pili  kupitia  zabuni. Sheria  mpya  ya  madini  sheria  namba  14  ya  2010 ndiyo  kiini  cha  makala  haya.

2.LESENI  KWA  MAOMBI  MAALUM.
Kwa  maombi  maalum  ni  hatua  ya  kawaida  ya  kuomba  kama ambavyo  unaweza  kuomba  kazi  au  tenda  yoyote  ambayo haijatangazwa na  serikali. Hatua  hii  huja  baada  ya  mjasiriamali  kuliona  eneo  la  madini   na  kuamini  kuwa  anaweza  kuwa  sehemu  ya  biashara  ya  eneo  hilo. 
Maombi  hufanywa  katika  fomu  maalum  ambazo   hupatikana  kwa  kamishna  wa  madini.  Makamishna  wa  madini  hupatikana  hata  wilayani  au  mikoani  hivyo  inategemea  ni  sehemu  ipi unataka  kutafuta  hayo  madini.
 Kubwa  ni  kuwa  utatakiwa  kutumia  wilaya  au  mkoa  husika  katika  kupata  fomu   hiyo  kwa  ajili  ya  kutuma  hayo  maombi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...