MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi, Abdallah Bulembo amesema anaguswa na kazi nzuri ya utekelezaji wa Ilani ya CCM inayofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda katika ujenzi wa shule za sekondari  za kata.
Bulembo ambaye pia ni Mjumbe wa kamati kuu ya CCM alisema kutokana na jitihada hizo ameona haja ya kumtia moyo DC Makonda kwa kuchangia ujenzi wa shule hizo saba unaoendelea.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa kukabidhi saruji mifuko 500 Bulembo alimtaka Makonda kuendelea kupigania utekelezaji wa Ilani bila kujali itikadi za vyama katika kuleta maendeleo ya wilaya hiyo.
Alisema Jumuiya ya wazazi kazi yake kubwa ni ulezi hivyo mafanikio yatakayopatikana kutokana na wanafunzi zaidi ya 3183 waliokosa shule katika wilaya hiyo kuweza kuendelea na masomo ni ya kujivunia.
Aliwataka watendaji wa Manispaa hiyo kuhakikisha malengo ya ujenzi huo yanatimia ili kuokoa watoto ambao wangeathirika kutokana na kukosa elimu.
Makonda aliwapongeza wote wanaojitokeza katika kumuunga mkono katika ujenzi wa shule hizo na kusema jana amepokea mifuko 1640 ya saruji.
Alisema saruji hiyo ni mifuko 500 kutoka kwa Bulembo, 500 kutoka kwa  Askofu Mkuu mstaafu  wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dk. Alex Malasusa na mifuko 640 kutoka Kampuni ya The Duma Group.
Aliwahakikishia wadau hao wa elimu kuwa atasimamia ipasavyo ujenzi wa shule hizo ili kupunguza wimbi la watoto wasio na elimu Kinondoni ambao ndio chimbuko la vijana wanaotumia dawa za kulevya,biashara ya ngono,vibaka,mimba za utotoni na wahalifu wengine.
Mkurugenzi wa Kampuni ya The Duma Group, Areeq Amran Mohamed alisema lengo la kusaidia saruji hiyo ni kuungana na serikali katika kutekeleza sera ya kuinua elimu wilaya ya Kinondoni.
Akiongea baada ya kupokea misaada hiyo, DC Makonda alisema:
"Napenda kumshukuru sana Baba Askofu Malasusa kwa kunichangia mifuko 500 ya cement kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa madarasa.  
"Pia namshukuru sana Mhe Abdallah Bulembo Mwenyekiti wa WAZAZI CCM  Taifa kwa support ya mifuko 500 ya cement na mwisho, si kwa Umuhimu,  bali kwa upande ni kampuni ya The Duma Group kwa mifuko 640 ya cement.  
"Naowaombea kwa Mungu awape maradufu kwani kitendo hiki ni kitendo cha kiungwana. Mmetuvisha nguo wanaKinondoni. Nawe mtanzania mwenzangu kama unamchango wowote bado nakukaribisha.



Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda akipokea mifuko 640 ya cement kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya The Duma Group, Bw. Areeq Amran Mohamed

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda akitoa shukurani kwa Mhe Abdallah Bulembo mwenyekiti wa wazazi ccm Taifa kwa mchango wake wa mifuko 500 ya Cement.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. KILA LA KHERI MAKONDA,UNAFANYA KAZI SAFI KABISA INAONEKANA ACHANA NA WANAOKUSEMA KWA UBAYA LAKINI KAZI YAKO INAONEKANA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...