Na Bashir Yakub
Adhabu hizi zimeainishwa kifungu cha 25 cha kanuni za adhabu sura ya 16. Ni adhabu zinazohusu makosa ya jinai.
1.ADHABU YA KIFO ( DEATH PENALTY).
Adhabu hii hutolewa kwa wenye makosa makubwa kama kuua kwa kukusudia(murder). Kifungu cha 26 kanuni za adhabu kinasema kuwa, mtu atakapohukumiwa adhabu ya kifo basi adhabu hiyo itatekelezwa kwa kunyongwa kwa kitanzi mpaka mtu huyo atakapokufa.
Hata hivyo adhabu hii hutekelezwa kwa namna tofauti katika nchi mbalimbali. Baadhi ya nchi adhabu ya kifo hutekelezwa kwa kupiga risasi na nyingine kudungwa sindano ya sumu. Sisi kwetu ni kitanzi/kamba shingoni kwa kuninginizwa mpaka roho itoke.
Pamoja na hayo adhabu hii inapingwa sana na mashirika ya haki za binadamu pamoja na wanaharakati wengine duniani kote.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...