Tokeo la picha la MAGEREZA

Na Bashir Yakub
Adhabu  hizi  zimeainishwa  kifungu  cha  25 cha  kanuni  za  adhabu  sura  ya 16. Ni  adhabu  zinazohusu  makosa  ya  jinai.

1.ADHABU  YA  KIFO ( DEATH PENALTY).

Adhabu  hii  hutolewa  kwa  wenye  makosa  makubwa  kama  kuua  kwa  kukusudia(murder).  Kifungu  cha  26  kanuni  za  adhabu  kinasema  kuwa,  mtu  atakapohukumiwa  adhabu  ya  kifo  basi  adhabu  hiyo itatekelezwa  kwa  kunyongwa  kwa  kitanzi  mpaka  mtu  huyo  atakapokufa.

Hata  hivyo  adhabu  hii  hutekelezwa  kwa  namna tofauti   katika nchi mbalimbali. Baadhi  ya nchi  adhabu  ya kifo  hutekelezwa  kwa  kupiga  risasi   na  nyingine  kudungwa  sindano  ya  sumu. Sisi  kwetu  ni  kitanzi/kamba  shingoni  kwa kuninginizwa mpaka roho  itoke. 

 Pamoja  na  hayo  adhabu  hii  inapingwa  sana  na  mashirika ya  haki  za  binadamu  pamoja  na  wanaharakati wengine duniani kote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...