Mkurugenzi wa Hospitali ya Walemavu CCBRT, Bi. Brenda Msangi akimueleza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai (kulia) kuhusu namna ya utendaji kazi hospitalini hapo. Spika alitembelea hospitali hiyo kuangalia utendaji kazi kama mlezi wao.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (mwenye tai nyekundu) akipokea machapisho yanayohusu masuala ya walemavu kutoka kwa Afisa Mtetezi CCBRT wa masuala ya walemavu, Bw. Fredrick Msigala wakati alipotembelea hospitali hiyo kwa mara ya kwanza akiwa ni Mlezi wa Hospitali hiyo.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia) akipata maelekezo juu ya namna ya wagonjwa wa macho wanavyowekewa macho bandia (artificial eyes) wakati alipotembelea hospitali hiyo kwa mara ya kwanza akiwa ni Mlezi wa Hospitali hiyo. Kulia ni ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mpoki Ulisubisya.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...