Mhe. Waziri wa Afya.Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumzia uzefu wa Tanzania katika kukabiliana na tatizo la  ukeketaji akiwa na wazungumzaji wengine katika Meza Kuu, kutoka kushoto ni Mke wa  Rais wa Burkina Faso Bi. Sika Bella Kabore,  Bw. Benoit Kalasi (UNFPA), Bi.Emma Bonino Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Italia.
  Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, Mhe. Peter Serukamba akifuatilia majadiliano kuhusu tatizo la  ukeketaji  na  adhari zake wa afya na maendeleo ya mtoto wa kike na mwanamke.
 Wajumbe kutoka Serikali ya Mapinduzi nao wakifuatilia majadiliano  yaliyovutia washiriki wengi kuhusu madhara  yatokanayo  na ukeketaji na namna gani  jamii inatakiwa kushirikiana kutokoza tatizo hilo. 
Sehemu ya washiriki wa Mkutano na majadiliano  kuhusu utokomezaji wa vitendo vya ukeketaji na uhusiano wake na utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu. Mkutano huu  uliandaliwa kwa pamoja na Wakilishi za  Kudumu za Tanzania, Burkina Faso, Italy, Iran, UNFPA na UNCEF.


Na Mwandishi Maalum, New York
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ( Mb)  amesisitiza   kuwa ni  kwa ushirikiano baina ya Serikali  na  jamii ndipo tatizo la ukeketaji  kwa watoto wa kike na wanawake litakapoweza kutokomezwa.

Akaongeza kwamba, serikali  inaweza kutunga sheria nyingi  za kukabiliana na tatizo hilo  lakini kama jamii yenyewe  kuanzia ngazi  ya familia isipotoa ushuriano wa dhani itachukua muda mrefu kwa tatizo hilo kutokomezwa. Alikuwa akizungumza wakati wa majadiliano ya mkutano wa  kuhusu  utokomezwaji  vitendo vya ukeketaji kama sehemu  muhimu ya utekelezaji wa Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu ( Agenda 2030.

Waziri Ummy Mwalimu alikuwa mmoja wa  wazungumzaji wakuu  katika  mkutano  huo  uliowahusisha  Mke wa Rais wa  Burkina Faso, Bibi. Sika Bella Kabore, Mawaziri na  Asasi za Kiraia na uliandaliwa kwa pamoja  na Wakilishi za kudumu za Tanzania,  Italy, Iran, Burkina Faso,UNFPA na UNICEF, ikiwa ni sehemu ya Mkutano wa 60 wa Kamisheni  ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Wanawake.

Na kwa sababu hiyo, Waziri  Ummy Mwalimu, amerejea kutoa wito kwa watanzania wote kwa  katika ujumla wao   wakiwamo wazee wa kimila, viongozi wa dini na vijana wakiume    kutoa ushirikiano kwa  serikali na wadau wengine ili hatimaye tatizo hilo ambalo   linaelezwa  kuwa  siyo tu lina madhara makubwa kiafya na kisaikolojia lakini pia ni ukiukwaji wa haki za binadamu.

“Tunatakiwa kufanya kazi kwa  pamoja na katika umoja  wetu, serikali peke yake haitaweza kulimaliza tatizo hili, ambalo  imefikia mahali  sasa  wazazi kwa kuongopa mkono wa sharia wanaamua kuwafanyia ukeketeji watoto wa kike katika umri  mdogo sana” Akaeleza Waziri.Akasema  , Tanzania  imebaini  uelimishwaji na  majadiliano  yanayohusisha familia na vijana wakiume ni muhumu katika kuchangiza juhudi za serikali katika  kukabili ukeketaji.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...