Watanzania wameaswa
kujenga tabia ya kujiwekea akiba kupitia mabenki kwa manufaa yao na taifa kwa
kwa ujumla ikiwa ni mchango wao katika kutekeleza kaulimbiu ya Mhe. Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ili kufikia malengo
waliojiwekea katika kujiletea maendeleo endelevu.
Hayo yamesemwa na Meneja wa Fedha na Utawala kutoka Bodi ya
Bima na Amana (DIB) iliyo chini ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Richard Malisa wakati
akitoa mada juu ya bodi hiyo katika semina ya waandishi wa habari iliyoandaliwa
na benki hiyo kwa lengo la kuwajengea uwezo waandishi hao katika kuandika, kutoa
na kusambaza habari za sekta ya uchumi biashara na fedha.
“Pesa zinapowekwa na kuwa benki hutumika kuchangia kuinua na
kuimarisha usalama wa akiba ya mtu binafsi na kwa upande wa nchi zinatumika
katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo kuinua sekta ya elimu, afya,
maji, ujenzi wa barabara na kilimo”
alisema Malisa.
Katika kuonesha umuhimu wa bodi hiyo nchini, Malisa alisema
kuwa taasisi ama mtu binafsi anapoweka pesa zake benki, hiyo ni amana kubwa na
muhimu kwa kuwa tabia hiyo ya uwekaji pesa ina tija na inaongeza usalama wa
pesa ambayo ni njia salama ikilinganishwa na kutumia njia za zamani za watu kuweka
pesa kwenye godoro ambayo sio salama.
Faida nyingine za mtu binafsi ama taasisi kuweka pesa zao
benki ni kuongeza mtaji wake kwa kupata riba kulingana na muda pesa hizo zinapokuwa
benki na mteja anauhakika pesa yake ipo salama kwa kuwa ipo mikononi mwa Bodi
ya Bima na Amana endapo litatokea tatizo lolote kwenye benki alipoweka pesa
zake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...